Hamia kwenye habari

Ndugu Sergey Kuznetsov

JANUARI 6, 2023 | HABARI ZILIONGEZWA: APRILI 19, 2023
URUSI

HABARI ZA KARIBUNI—NDUGU AHUKUMIWA | “Ninaendelea Kumtumaini Yehova Hata Zaidi”

HABARI ZA KARIBUNI—NDUGU AHUKUMIWA | “Ninaendelea Kumtumaini Yehova Hata Zaidi”

Aprili 18, 2023, Mahakama ya Jiji la Nevinnomyssk katika Eneo la Stavropol ilimhukumu Ndugu Sergey Kuznetsov kifungo cha nje cha miaka sita. Hahitaji kwenda gerezani wakati huu.

Maelezo Mafupi Kumhusu

Yehova amemtunza sana Sergey na hilo linatuhakikishia kwamba anaona ‘taabu zetu zote’ naye ‘atatwinua na kutubeba’ tunapokabili jaribu lolote.​—Isaya 63:9.

Mfuatano wa Matukio

  1. Novemba 21, 2018

    Wenye mamlaka walivamia nyumba nyingi za Mashahidi huko Nevinnomyssk, kutia ndani nyumba ya Sergey

  2. Desemba 12, 2019

    Kesi ya uhalifu yafunguliwa

  3. Juni 18, 2020

    Aongezwa kwenye orodha ya watu wenye msimamo mkali

  4. Mei 31, 2022

    Awekewa vizuizi vya kusafiri

  5. Septemba 7, 2022

    Kesi ya uhalifu yaanza