Hamia kwenye habari

Ndugu Aleksey Kupriyanov akiwa na mke wake, Yelena

FEBRUARI 16, 2023| HABARI ZIMEONGEZWA: SEPTEMBA 21, 2023
URUSI

HABARI ZA KARIBUNI—NDUGU AMEFUNGUWA | ‘Ninathamini Hata Zaidi Maandalizi ya Yehova’

HABARI ZA KARIBUNI—NDUGU AMEFUNGUWA | ‘Ninathamini Hata Zaidi Maandalizi ya Yehova’

Septemba 15, 2023, Mahakama ya Jiji la Kovrovskiy iliyo katika Eneo la Vladimir ilimhukumu Ndugu Aleksey Kupriyanov kifungo cha mwaka mmoja gerezani. Hata hivyo, kutokana na muda ambao tayari alitumia mahabusu na katika kifungo cha nyumbani, inahesabiwa kwamba amekamilisha kifungo chake. Hatahitaji kwenda gerezani wakati huu.

Maelezo Mafupi Kumhusu

Sisi pia tumeazimia kutumia maandalizi tunayopata kutoka kwa Yehova ambayo yanatusaidia “[kuvaa] mavazi kamili ya silaha . . . ili [tuweze] kusimama imara dhidi ya matendo yenye hila ya Ibilisi.”​—Waefeso 6:11.

Mfutano wa Matukio

  1. Februari 17, 2021

    Maofisa wa polisi walifanya msako katika nyumba saba za Mashahidi wa Yehova, kutia ndani nyumba ya familia ya Kupriyanov. Ndugu na dada ishirini na watatu walihojiwa.

  2. Juni 28, 2021

    Kesi ya uhalifu ilifunguliwa. Aleksey alishtakiwa kwa sababu ya kushiriki utendaji wa shirika lenye msimamo mkali hasa kuhudhuria mikutano

  3. Julai 8, 2021

    Nyumba yao ilifanyiwa msako kwa mara ya pili. Alihojiwa na kuwekwa kizuizini

  4. Julai 9, 2021

    Alihamishwa na kupelekwa mahabusu

  5. Novemba 19, 2021

    Alitolewa mahabusu na kuwekwa chini ya kifungo cha nyumbani

  6. Juni 21, 2022

    Alipewa ruhusa ya kutoka nyumbani lakini aliwekewa vizuizi vingine kuhusiana na sehemu anazoweza kwenda na mambo anayoweza kufanya

  7. Oktoba 4, 2022

    Kesi ya uhalifu ilianza