MEI 18, 2022 | HABARI ZIMEONGEZWA: MACHI 12, 2024
URUSI
HABARI ZA KARIBUNI—NDUGU AMEFUNGWA | Inver Siyukhov Ajazwa Nguvu
Machi 7, 2024, Mahakama ya Jiji la Maykop iliyo katika Jamhuri ya Adygeya ilimhukumu Ndugu Inver Siyukhov kifungo cha miaka sita gerezani. Amekuwa mahabusu tangu Aprili 2021 naye ataendelea kubaki kizuizini.
Mfuatano wa Matukio
Aprili 15, 2021
Alishtakiwa kwamba aliendesha mkutano mtandaoni
Aprili 16, 2021
Wenye mamlaka walifanya msako kwenye nyumba ya Inver na pia kwenye nyumba za Mashahidi wengine wanne wa Yehova. Alihojiwa na kuwekwa kizuizini
Aprili 17, 2021
Alipelekwa mahabusu
Agosti 15, 2021
Alihamishwa na kupelekwa kwenye gereza lenye ulinzi mkali lililo kilometa 110 kutoka Maykop
Septemba 13, 2021
Kesi ya uhalifu ilianza
Maelezo Mafupi Kumhusu
Tuna hakika kwamba ndugu na dada zetu wapendwa walio Urusi wataendelea “kujipatia nguvu katika Bwana na katika uwezo wa nguvu zake.”—Waefeso 6:10.
a Kwa kuwa kwa sasa Ndugu Siyukhov yuko mahabusu, hatukuweza kupata maelezo kutoka kwake.