JULAI 26, 2022 | HABARI ZIMEONGEZWA: DESEMBA 6,
URUSI
HABARI ZA KARIBUNI—NDUGU WAHUKUMIWA | Sala Inawaimarisha
Desemba 5, 2023
Mahakama ya Jiji la Surgut iliyo katika Eneo Lililotengwa la Khanty-Mansi—Yugra iliwahukumu ndugu 17 pamoja na dada mmoja. Miongoni mwao ni Ndugu Vyacheslav Boronos, Ndugu Saveliy Gargalyk, Ndugu Yevgeniy Kayryak, Ndugu Artem Kim, Ndugu Sergey Loginov, Ndugu Aleksey Plekhov, na Ndugu Sergey Volosnikov. Ndugu hao 17 walihukumiwa kifungo cha nyumbani cha kati ya miaka sita na miezi mitatu na miaka saba. Dada alihukumiwa kifungo cha nyumbani cha miaka mitatu na miezi mitatu. Hawahitaji kwenda gerezani wakati huu.
Mfuatano wa Matukio
Februari 15, 2019
Maofisa wa polisi walifanya msako kwenye nyumba nyingi za Mashahidi wa Yehova jijini Surgut na pia katika majiji yaliyo karibu. Baada ya msako huo, ndugu watatu kutia ndani Sergey Loginov, waliwekwa mahabusu. Baadaye ndugu mwingine aliagizwa kwenda kwenye hospitali ya watu wenye matatizo ya kiakili. Ndugu saba wanaotajwa kwenye ripoti hii waliteswa baada ya kukataa kutoa habari kuwahusu waabudu wenzao
Februari 26, 2019
Mahakama ya Ulaya ya Haki za Kibinadamu iliagiza serikali ya Urusi imwachilie Sergey Loginov ili apate matibabu
Aprili 11, 2019
Sergey Loginov aliachiliwa kutoka mahabusu
Oktoba 29, 2021
Kesi ya uhalifu ilianza
Maelezo Mafupi Kuwahusu
Ndugu zetu wenye ujasiri wanapoendelea kukabiliana na majaribu, tuna uhakika kwamba Yehova anasikiliza sala zao na kuwajibu haraka wanapotaabika.—Zaburi 69:17.