Hamia kwenye habari

Kushoto hadi kulia: Ndugu Rinat Kiramov na mke wake, Galina; Ndugu Sergey Korolev na mke wake, Yekaterina; na Ndugu Sergey Kosyanenko na mke wake, Olga

MACHI 29, 2023 | HABARI ZILIONGEZWA: APRILI 18, 2023
URUSI

HABARI ZA KARIBUNI—NDUGU WANAFUNGWA | Yehova Anawasaidia Ndugu Zetu Gerezani

HABARI ZA KARIBUNI—NDUGU WANAFUNGWA | Yehova Anawasaidia Ndugu Zetu Gerezani

Aprili 17, 2023, Mahakama ya Wilaya ya Ahktubinskiy iliyo katika Eneo la Astrakhan iliwahukumu Ndugu Rinat Kiramov, Ndugu Sergey Korolev, na Ndugu Sergey Kosyanenko kifungo cha miaka saba gerezani kila mmoja. Ndugu wote watatu wamekuwa mahabusu tangu Novemba 2021 na wamebaki humo.

Maelezo ya Kibinafsi

Tunafarijika kujua kwamba Yehova anaendelea kuthibitisha yeye ni kimbilio la watumishi wake waaminifu na kwamba ameweka ‘mikono yake ya milele chini yetu.’​—Kumbukumbu la Torati 33:27.

Mfuatano wa Matukio

  1. Novemba 9, 2021

    Kesi ya uhalifu ilifunguliwa. Maofisa wa polisi walifanya msako kwenye nyumba 15 za Mashahidi wa Yehova zilizo Akhtubinsk na Znamensk, kutia ndani nyumba za Ndugu Kiramov, Ndugu Korolev, na Ndugu Kosyanenko

  2. Novemba 10, 2021

    Sergey Korolev alikamatwa

  3. Novemba 11, 2021

    Rinat Kiramov na Sergey Kosyanenko walikamatwa. Ndugu hao wote watatu walipelekwa mahabusu

  4. Novemba 14, 2022

    Kesi ya uhalifu ilianza

a b Hatukuweza kupata maelezo kutoka kwa Ndugu Kiramov na Ndugu Kosyanenko.