Hamia kwenye habari

Kuanzia kulia kwenda kushoto: Ndugu Aleksandr Akopov, Ndugu Konstantin Samsonov, Ndugu Shamil Sultanov

JUNI 2, 2021
URUSI

HABARI ZA KARIBUNI | Ndugu Akopov, Ndugu Samsonov, na Ndugu Sultanov Waendelea Kumtegemea Yehova Kesi Yao Inapoendelea

HABARI ZA KARIBUNI | Ndugu Akopov, Ndugu Samsonov, na Ndugu Sultanov Waendelea Kumtegemea Yehova Kesi Yao Inapoendelea

Aprili 19, 2022, Mahakama ya Wilaya ya Neftekumskiy iliyo katika Eneo la Stavropol iliwahukumu Ndugu Aleksandr Akopov, Ndugu Konstantin Samsonov, na Ndugu Shamil Sultanov. Aleksandr na Shamil walitozwa faini ya rubo 500,000 (dola 6,055 za Marekani) kila mmoja. Hawatahitaji kulipa faini hizo kwa sababu ya muda ambao wamekuwa mahabusu. Konstantin alihukumiwa kifungo cha miaka saba na nusu gerezani. Alipelekwa kizuizini mara moja.

Maelezo mafupi kuwahusu

Aleksandr Akopov

  • Alizaliwa: 1992 (Neftekumsk)

  • Maisha Yake: Anafanya kazi ya ujenzi pamoja na baba yake na kaka yake. Anapenda kucheza mpira wa miguu, mpira wa kikapu, tenisi, kutembelea maeneo ya asili, na kupika

    Alibatizwa kuwa Shahidi wa Yehova mwaka wa 2007 akiwa na umri wa miaka 14

Konstantin Samsonov

  • Alizaliwa: 1977 (Neftekumsk)

  • Maisha Yake: Alipokuwa kijana alipenda mchezo wa chess na teknolojia ya kompyuta. Kwa sasa anafanya kazi akiwa mhandisi wa mitambo katika hospitali. Yeye pamoja na mke wake, Svetlana walianza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova katika mwaka wa 1998. Walibatizwa mwaka 2000. Wana mwana mmoja

Shamil Sultanov

  • Alizaliwa: 1977 (Mahmud-Mekteb, Eneo la Stavropol)

  • Maisha Yake: Anadumisha na kurekebisha majengo. Alijifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova katika mwaka wa 2000 hivi. Alibatizwa mwaka wa 2003, Alifunga ndoa na Elena mwaka 2004. Alimsaidia kumlea mwana wake aliyempata katika ndoa yake ya awali

Historia ya Kesi

Jumamosi ya Agosti 26, 2017, polisi wenye silaha waliwazunguka Mashahidi wa Yehova 18 walioenda kufurahia likizo karibu na ziwa lililo karibu na Neftekumsk. Kikundi hicho kilichotia ndani watoto na wazee-wazee kilichukuliwa kwa basi na kupelekwa katika kituo cha polisi ambapo walihojiwa kwa muda wa saa tatu. Baada ya hapo, ndugu na dada wengi walio Neftekumsk waliwekwa chini ya uchunguzi na pia nyumba zao zilifanyiwa msako. Ndugu Aleksandr, Ndugu Konstantin, na Ndugu Shamil waliwekwa kizuizini kwa karibu mwaka mzima.

Aleksandr anakiri kwamba aliogopa kufungwa kwa sababu anakabiliana na tatizo la wasiwasi mwingi na ana matatizo ya kiafya. Alisali sana na kumwomba Yehova amsaidie kiakili na kihisia ili aweze kuvumilia gerezani. Anasema hivi: “Mara nyingi nilimwambia Yehova kwamba nisingeweza kuendelea, siamini kwamba niliweza kuvumilia karibu mwaka mzima nikiwa mahabusu.” Yehova alijibu sala zake kwa kumsaidia kukumbuka mistari ya Biblia wakati ambapo hakuwa na Biblia yenyewe. Aliandika kila mstari aliyoukumbuka, akapitia mstari moja kila asubuhi na kufikiria mstari huo unawezaje kumsaidia katika hali yake. Hili lilimsaidia kuona kifungo chake kupitia macho ya Yehova.

Ujasiri wa Konstantin uliongezeka kupitia barua nyingi alizopokea kutoka kwa mke wake. Katika barua moja, mke wake alipendekeza kwamba aone majaribu yake kama jambo watu wanafanya mara mojamoja ili kujifurahisha. Anasema hivi: “Jambo hilo lilinifurahisha, na baadaye kwa kweli mambo yalikuwa rahisi zaidi.”

Shamil anasema kwamba miezi kadhaa ya kwanza niliyokuwa mahabusu ilikuwa ngumu sana kwangu. Anasema hivi: “Baada ya muda kukawa na afadhali, na huu ulikuwa uthibitisho wa kwamba sikuwa nimeachwa peke yangu.” Katika kipindi hiki, alijifunza kumtumaini Yehova zaidi bila kuwa na wasiwasi mwingi kwa sababu ya majaribu ambayo angeendelea kukabili.

Ndugu wote watatu wamewekewa vikwazo vya kusafiri na hawawezi kutumia simu wala Intaneti. Vizuizi hivi vinafanya iwe vigumu kwa Aleksandr kupata matibabu anayohitaji na vinamzuia Konstantin kufanya kazi yake ya uhandisi wa mitambo wa kompyuta. Lakini licha ya changamoto hizi, ndugu hao wameazimia kubaki wakiwa waaminifu kwa Mungu wao.

Tunajua kwamba Yehova atawabariki ndugu hawa kadiri wanavyoendelea kumtegemea yeye.​—Zaburi 20:7.