AGOSTI 5, 2021
URUSI
HABARI ZA KARIBUNI | Ndugu Dmitriy Terebilov Anakabili Kifungo kwa Mara ya Tano, Lakini Mara ya Kwanza kwa Sababu ya Imani Yake
Septemba 22, 2022, Mahakama ya Pili ya Kuchunguza Upya Maamuzi ya Mahakama za Chini ya Urusi ilikataa ombi la pili la rufaa la Ndugu Dmitriy Terebilov. Bado yuko gerezani.
Januari 12, 2022, Mahakama ya Eneo la Kostroma ilikataa ombi la rufaa la Dmitriy.
Mfuatano wa Matukio
Septemba 6, 2021
Mahakama ya Wilaya ya Sverdlovskiy katika jiji la Kostroma ilimhukumu Dmitriy kifungo cha miaka mitatu gerezani. Alipelekwa gerezani moja kwa moja baada ya hukumu kutangazwa
Septemba 8, 2020
Kesi ya uhalifu dhidi ya Dmitriy inaanza
Mei 25, 2020
Dmitriy anashtakiwa rasmi na kuwekewa vizuizi vya kusafiri
Septemba 19, 2019
Pesa zilizo katika akaunti ya benki ya Dmitriy zinazuiliwa
Juni 13, 2019
Kesi ya uhalifu inafunguliwa dhidi ya Dmitriy kwa sababu ya kugawa machapisho yaliyopigwa marufuku na kushiriki katika mikutano ya shirika lililopigwa marufuku
Julai 25, 2018
Nyumba ya Dmitriy inafanyiwa upekuzi yeye na mke wake walipokuwa njiani kutoka kusanyiko la eneo nchini Moldova. Maofisa waliwazuilia na kuwahoji mara tu waliporudi nyumbani
Maelezo Mafupi Kumhusu
Dmitriy anaendelea kuwa na shangwe inayotokana na ‘kushutumiwa kwa ajili ya jina la Kristo,’ nasi tuna uhakika kwamba “roho ya utukufu, yaani roho ya Mungu, inatulia juu” yake.—1 Petro 4:14.