Hamia kwenye habari

Ndugu Andrey Zhukov

JUNI 7, 2022 | HABARI ZIMEONGEZWA: NOVEMBA 21, 2023
URUSI

HABARI ZA KARIBUNI—UAMUZI WABADILISHWA | Andrey Anasadiki Kwamba Yehova Anampenda na Anamtegemeza

HABARI ZA KARIBUNI—UAMUZI WABADILISHWA | Andrey Anasadiki Kwamba Yehova Anampenda na Anamtegemeza

 

Novemba 20, 2023, Mahakama ya Eneo Lililotengwa la Khanty-Mansi ilibadili uamuzi wa kumwondolea mashtaka Ndugu Andrey Zhukov. Kesi yake itarudishwa ili kusikilizwa tena.Mahakama ya Wilaya ya Yugorskiy iliyo katika Eneo Lililotengwa la Khanty-Mansi—Yugra imebatilisha uamuzi wake katika kesi inayomhusu Ndugu Andrey Zhukov. Hakupatikana na hatia yoyote kwa mashtaka yote yaliyokuwa yakimkabili.

Mfuatano wa Matukio

  1. Agosti 17, 2020

    Wenye mamlaka walifungua kesi ya uhalifu dhidi ya Andrey kwa madai ya kwamba alikuwa akiongoza mikutano ya siri ya shirika “lenye msimamo mkali”

  2. Agosti 19, 2020

    Nyumba tisa za Mashahidi wa Yehova zilivamiwa kutia ndani nyumba ya Andrey. Aliwekwa kizuizini

  3. Agosti 20, 2020

    Aliachiliwa lakini akawekewa vizuizi

  4. Januari 14, 2021

    Andrey aliwekwa kwenye orodha ya watu wenye msimamo mkali, na akaunti yake ya benki ikazuiliwa

  5. Agosti 4, 2021

    Wenye mamlaka waliongeza mashtaka dhidi ya Andrey. Mashtaka hayo yalitia ndani, “kusali kwa Yehova Mungu, kufanya mikutano wa kidini, na kusoma machapisho ya kidini.” Baadaye alihojiwa

  6. Oktoba 15, 2021

    Maombi ya kukomesha kesi hiyo yalikataliwa

  7. Desemba 29, 2021

    Kesi ilianza

Maelezo Mafupi Kumhusu

Utegemezo ambao Yehova anampa Andrey na ndugu na dada zetu wapendwa wanaokabili upinzani ni‘uthibitisho wa wema wake’ na unaonyesha waziwazi kwamba Yehova ni ‘msaidizi na mfariji wetu.’​—Zaburi 86:17; maelezo ya chini.