JUNI 7, 2022 | HABARI ZIMEONGEZWA: NOVEMBA 21, 2023
URUSI
HABARI ZA KARIBUNI—UAMUZI WABADILISHWA | Andrey Anasadiki Kwamba Yehova Anampenda na Anamtegemeza
Novemba 20, 2023, Mahakama ya Eneo Lililotengwa la Khanty-Mansi ilibadili uamuzi wa kumwondolea mashtaka Ndugu Andrey Zhukov. Kesi yake itarudishwa ili kusikilizwa tena.Mahakama ya Wilaya ya Yugorskiy iliyo katika Eneo Lililotengwa la Khanty-Mansi—Yugra imebatilisha uamuzi wake katika kesi inayomhusu Ndugu Andrey Zhukov. Hakupatikana na hatia yoyote kwa mashtaka yote yaliyokuwa yakimkabili.
Mfuatano wa Matukio
Agosti 17, 2020
Wenye mamlaka walifungua kesi ya uhalifu dhidi ya Andrey kwa madai ya kwamba alikuwa akiongoza mikutano ya siri ya shirika “lenye msimamo mkali”
Agosti 19, 2020
Nyumba tisa za Mashahidi wa Yehova zilivamiwa kutia ndani nyumba ya Andrey. Aliwekwa kizuizini
Agosti 20, 2020
Aliachiliwa lakini akawekewa vizuizi
Januari 14, 2021
Andrey aliwekwa kwenye orodha ya watu wenye msimamo mkali, na akaunti yake ya benki ikazuiliwa
Agosti 4, 2021
Wenye mamlaka waliongeza mashtaka dhidi ya Andrey. Mashtaka hayo yalitia ndani, “kusali kwa Yehova Mungu, kufanya mikutano wa kidini, na kusoma machapisho ya kidini.” Baadaye alihojiwa
Oktoba 15, 2021
Maombi ya kukomesha kesi hiyo yalikataliwa
Desemba 29, 2021
Kesi ilianza
Maelezo Mafupi Kumhusu
Utegemezo ambao Yehova anampa Andrey na ndugu na dada zetu wapendwa wanaokabili upinzani ni‘uthibitisho wa wema wake’ na unaonyesha waziwazi kwamba Yehova ni ‘msaidizi na mfariji wetu.’—Zaburi 86:17; maelezo ya chini.