Hamia kwenye habari

Ndugu Aleksandr Tsikunov

DESEMBA 6, 2023
URUSI

“Hakuna Jaribu Linaloweza Kuvunja Imani ya Kweli”

“Hakuna Jaribu Linaloweza Kuvunja Imani ya Kweli”

Mahakama ya Wilaya ya Kaltanskiy iliyo katika Eneo la Kemerovo itatangaza uamuzi wake hivi karibuni katika kesi inayomhusu Ndugu Aleksandr Tsikunov. Mwendesha-mashtaka bado hajatoa ombi la hukumu anayopendekeza.

Maelezo Mafupi Kumhusu

Tunafurahi kuwa na vielelezo vingi vya watu washikamanifu wanaotukumbusha kwamba yeyote anayemwamini Yehova na Mwana wake, Yesu Kristo, hatakata tamaa.​—Waroma 10:11.

Mfuatano wa Matukio

  1. Aprili 27, 2021

    Kesi ya uhalifu ilifunguliwa

  2. Mei 2, 2021

    Nyumba ilifanyiwa msako. Alikamatwa na kupelekwa mahabusu

  3. Mei 4, 2021

    Alitolewa mahabusu na kuwekwa katika kifungo cha nyumbani

  4. Juni 24, 2021

    Aliachiliwa kutoka katika kifungo cha nyumbani na kuwekewa vizuizi vya kusafiri

  5. Julai 25, 2023

    Kesi ya uhalifu ilianza