FEBRUARI 20, 2023
URUSI
“Maadamu Yehova Yuko Pamoja Nami, Sikuzote Nitajihisi Nikiwa Nyumbani”
Februari 17, 2023, Mahakama ya Jiji la Gorno-Altayskiy iliyo katika Jamhuri ya Altai ilimhukumu Ndugu Aleksandr Kalistratov kifungo cha nje cha miaka sita na nusu. Hahitaji kwenda gerezani wakati huu.
Maelezo Mafupi Kumhusu
Tuna uhakika kwamba Yehova ataendelea kusikiliza sauti za watumishi wake waaminifu wanapomwita katika nyakati za taabu.—2 Samweli 22:7.
Mfuatano wa Matukio
2000
Alikamatwa kwa sababu ya kukataa kujiunga na utumishi wa kijeshi. Alikaa mahabusu kwa siku 21. Baadaye mahakama iliamua kwamba hana hatia
2010
Alishtakiwa kwa madai kwamba alikuwa na msimamo mkali. Kesi yake ilisikilizwa mara mbili kisha ikapelekwa kwenye Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Altai ambayo iliamua kwamba hana hatia
Desemba 16, 2021
Kesi ya uhalifu ilifunguliwa
Januari 16, 2022
Maofisa wa FSB walifanya msako katika nyumba tano za Mashahidi wa Yehova katika Jamhuri ya Altai. Maofisa hao walivamia nyumba ya Kalistratov na kumchukua Aleksandr ili kumhoji. Aliachiliwa siku hiyohiyo jioni na kuwekewa vizuizi vya kusafiri
Agosti 25, 2022
Kesi ya uhalifu ilianza