MEI 31, 2021
URUSI
Mahakama ya Urusi Yakataa Rufaa ya Mashahidi Wanne
Mei 28, 2021, Mahakama ya Mkoa wa Omsk ilikataa rufaa ya Ndugu Sergey Polyakov na mke wake, Anastasia, na pia ya Dada Gaukhar Bektemirova na Dada Dinara Dyusekeyeva. Ni lazima Ndugu Polyakov akae gerezani, na dada hao watatu wataendelea na vifungo vyao vya nje.