Hamia kwenye habari

NOVEMBA 24, 2020
URUSI

Mahakama ya Urusi Yamhukumu Ndugu Sergey Ledenyov Miaka Miwili ya Kifungo cha Nje

Mahakama ya Urusi Yamhukumu Ndugu Sergey Ledenyov Miaka Miwili ya Kifungo cha Nje

Novemba 24, 2020, Mahakama ya Jiji la Petropavlovsk-Kamchatskiy ya Eneo la Kamchatka ilimhukumu Ndugu Sergey Ledenyov. Alipewa kifungo cha nje cha miaka miwili, amekuwa kizuizini kwa miaka mitatu. Kwa sasa hahitaji kwenda gerezani.

Siku ya mwisho ya kesi, Sergey alieleza kwa ujasiri kinachomaanishwa na kuwa Shahidi wa Yehova. Alisema hivi: “Yehova si jina la watu, shirika, au imani. Yehova ndilo jina la kibinafsi la Mungu. Katika Biblia, kwenye kitabu cha nabii Isaya, Yehova anawaita watumishi wake waaminifu ‘mashahidi wangu.’ Kwa kutegemea maneno hayo, kwenye kusanyiko la mwaka 1931, walikubali jina ‘Mashahidi wa Yehova.’ Jina hilo linawakilisha mgawo wa kuwa mashahidi wa Mungu, yaani, kuwaambia wengine kumhusu yeye akiwa Muumba, Mwokozi, na Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu wote na kuhusu kusudi lake tukufu kwa mwanadamu. Hilo ni pendeleo kubwa kwangu na kwa waamini wenzangu.”—Isaya 43:10.

Kwa usadikisho mkubwa, Sergey aliiambia mahakama hivi: “Sina sababu ya kuaibika, kwa sababu sijatenda uhalifu wowote. Dhamiri yangu ni safi mbele za Mungu na wanadamu.”