Hamia kwenye habari

DESEMBA 16, 2020
URUSI

Mahakama ya Urusi Yamhukumu Ndugu Yuriy Savelyev Kifungo cha Miaka Sita Gerezani

Mahakama ya Urusi Yamhukumu Ndugu Yuriy Savelyev Kifungo cha Miaka Sita Gerezani

Desemba 16, 2020, Mahakama ya Wilaya ya Leninskiy huko Novosibirsk ilimhukumu Ndugu Yuriy Savelyev kifungo cha miaka sita gerezani. Ndugu yetu mpendwa, Yuriy, bado ni imara na anaendelea kujipatia ujasiri kwa kujifunza unabii wa Biblia katika funzo lake la kibinafsi.

Siku ya Desemba 9, Yuriy alitumia maelezo yake ya kumalizia akiwa mahakamani kutoa ushahidi kwa ujasiri. Alisema hivi mbele ya wote waliokusanyika: “Unabii ambao Yesu Kristo alitoa unatimia sasa hivi mbele ya macho yenu. Unapatikana katika Maandiko Matakatifu, Biblia, kwenye Marko 13:9, inaposema hivi: ‘Lakini ninyi jihadharini. Watu watawapeleka mahakamani, nanyi mtapigwa katika masinagogi na kusimamishwa mbele ya magavana na wafalme kwa ajili yangu, ili kuwa ushahidi kwao.’”