Hamia kwenye habari

Mei 18, 2020
URUSI

Maofisa wa Marekani Waandika Pendekezo la Kuomba Urusi Imwachilie Ndugu Dennis Christensen

Maofisa wa Marekani Waandika Pendekezo la Kuomba Urusi Imwachilie Ndugu Dennis Christensen

Washiriki wawili wa Bunge la Wawakilishi la Marekani, ambalo ni sehemu ya kisheria ya serikali ya Marekani, wamefikisha Azimio Na. 958 bungeni

linalotia ndani shutuma dhidi ya serikali ya Urusi kwa kumfunga isivyo haki Ndugu Dennis Christensen. Azimio hilo ndio hati ya karibuni zaidi kutoka kwa maofisa inayoshutumu Urusi kwa kuwatesa ndugu na dada zetu kwa sababu ya imani yao ya kidini.

Ndugu Christensen alikamatwa na kufungwa mnamo Mei 2017 kwa sababu ya kushiriki katika mikutano ya Kikristo ya Mashahidi wa Yehova. Azimio hilo, lililotolewa Mei 8, 2020 na Mwakilishi Eliot L. Engel na Michael T. McCaul, linaisihi serikali ya Urusi imwachilie mara moja Ndugu Christensen.

Azimio hilo linasema hivi: “Februari 6, 2019, Dennis Christensen, Shahidi wa Yehova na raia wa Denmark, alihukumiwa kifungo cha miaka sita gerezani. Tume ya Marekani ya Uhuru wa Kidini wa Kimataifa inashutumu uamuzi huo, na kuuona kuwa uthibitisho wa ziada unaoonyesha kwamba serikali ya Urusi imekuwa ikijihusisha au kukubaliana na uvunjaji mkubwa wa uhuru wa kidini.’”

Kufikia Mei 25, 2020, Ndugu Christensen atakuwa amefungwa gerezani kwa miaka mitatu. Yeye ni mmoja kati ya ndugu na dada 32 ambao wamekamatwa nchini Urusi, 9 tayari wamefungwa na 23 wako mahabusu wakisubiri kesi yao isikilizwe. Ndugu na dada wengine 18 wako katika kifungo cha nyumbani. Tangu 2017, maofisa wa Urusi wamevamia karibu nyumba 900 za ndugu zetu. Kwa sababu hiyo, Mashahidi 331 wa Yehova wafunguliwa mashtaka ya uhalifu.

Maofisa wa serikali nchini Marekani na barani Ulaya wameipinga Urusi vikali kwa sababu ya kuwatesa kidini Mashahidi wa Yehova.

Iwe Azimio Na. 958 litakubaliwa na kutokeza mabadiliko au la, tunajua kwamba Yehova ataendelea kuwasaidia ndugu na dada zetu nchini Urusi kuvumilia kwa shangwe. Tunatarajia wakati ambapo Yehova atawaondoa wote ‘wanaotunga matatizo kwa kutumia sheria.’—Zaburi 94:20-23.