Hamia kwenye habari

Ndugu Igor Avramenko, ambaye alikufa hivi karibuni, akiwa na mke wake Yelena

MACHI 30, 2020
URUSI

Maofisa wa Usalama wa Taifa (FSB) Wavamia na Kusababisha Uharibifu Mkubwa Katika Nyumba ya Ndugu Ambaye Alikufa Siku Kadhaa Kabla

Maofisa wa Usalama wa Taifa (FSB) Wavamia na Kusababisha Uharibifu Mkubwa Katika Nyumba ya Ndugu Ambaye Alikufa Siku Kadhaa Kabla

Machi 23, 2020, huko Khabarovsk Urusi, siku sita baada ya kifo cha Ndugu Igor Avramenko, Maofisa wa Usalama wa Taifa (FSB) walivamia nyumba yake bila huruma na kusababisha uharibifu mkubwa. Ndugu Avramenko alikufa kwa sababu ya tatizo la moyo. Maofisa hao walimwonyesha mke wa Ndugu  Avramenko, anayeitwa Yelena, kibali cha kufanya msako huo kilichokuwa na jina la Ndugu Avramenko. Licha ya hilo walichukua kompyuta, kamera, pamoja na vitu vingine vya dada huyo mjane.

Mapema siku hiyohiyo, maofisa wa usalama walienda kazini kwa Dada Avramenko na kumchukua hadi nyumbani, ambapo kiongozi wa msako huo, Stanislav Grebenkin, alimwonyesha kibali cha msako huo. Dada Avramenko alimweleza Bw Grebenkin kwamba mume wake amekufa. Alijua jambo hilo ila akajitetea kwamba kibali cha kufanya msako huo kilitolewa na wenye mamlaka kabla ya kufahamu kuhusu kifo cha mume wake, Ndugu Avramenko.

Ofisa huyo alimhakikishia Dada Avramenko kwamba maofisa hawatafanya msako mkubwa, akisema kwamba ilikuwa lazima wafanye hivyo ili “kesi ikamilishwe mapema na nyaraka zote zihifadhiwe na Maofisa wa Usalama wa Taifa.” Hata hivyo, walianza kufanya msako mkubwa na kuleta uharibifu mkubwa katika nyumba yake.

Katika eneo la Khabarovsk, jumla ya ndugu na dada 10 wamefunguliwa kesi za makosa ya kihalifu. Ijapokuwa wenye mamlaka wameendelea kujaribu kuwafanya ndugu na dada zetu wakane imani yao nchini Urusi, tunajua kwamba ‘watakuwa na nguvu wakiendelea kuwa watulivu na kuwa na tumaini’ katika Baba yetu mwenye upendo, Yehova.—Isaya 30:15.