FEBRUARI 5, 2024
URUSI
“Mkabidhi Yehova Njia Yako”
Mahakama ya Wilaya ya Shadrinskiy iliyo katika Eneo la Kurgan itatangaza uamuzi wake hivi karibuni katika kesi inayomhusu Ndugu Aleksandr Lubin. Mwendesha-mashtaka bado hajatoa ombi la hukumu anayopendekeza.
Maelezo Mafupi Kumhusu
Tuna uhakika kwamba kama Aleksandr, hata iwe tutakabili hali gani, tunaweza kuvumilia majaribu kwa uaminifu huku tukitegemea msaada wa Yehova.—Isaya 38:14.
Mfuatano wa Matukio
Julai 13, 2021
Kesi ya uhalifu ilianzishwa
Julai 14, 2021
Nyumba nane za Mashahidi wa Yehova zilifanyiwa msako. Aleksandr alikamatwa, akahojiwa, na kuwekwa kizuizini
Julai 16, 2021
Alisafirishwa na kupelekwa mahabusu
Julai 19, 2021
Alikata rufaa kwa sababu ya hali mbaya ya afya
Agosti 28, 2021
Baada ya Mahakama ya Umoja wa Ulaya ya Haki za Kibinadamu na mashirika ya haki za binadamu kuomba aachiliwe, Aleksandr aliachiliwa na kuwekewa vizuizi vya kusafiri
Julai 14, 2023
Kesi ya uhalifu ilianza
Septemba 7, 2023
Kesi iliahirishwa kwa sababu Aleksandr alikuwa amelazwa