Hamia kwenye habari

Ndugu Denis Antonov na mke wake, Olga (kushoto), na Ndugu Aleksandr Korolev na mke wake, Natalya (kulia), muda mfupi baada ya ndugu hao kuachiliwa kutoka gerezani

JUNI 19, 2024
URUSI

Ndugu Denis Antonov na Ndugu Aleksandr Korolev Wameachiliwa kutoka Gerezani Nchini Urusi

Ndugu Denis Antonov na Ndugu Aleksandr Korolev Wameachiliwa kutoka Gerezani Nchini Urusi

Juni 14, 2024, Ndugu Denis Antonov na Ndugu Aleksandr Korolev waliachiliwa kutoka katika gereza lililo katika kijiji cha Molochnitsa nchini Urusi. Agosti 25, 2022, ndugu wote wawili walihukumiwa kifungo cha miaka miwili gerezani. Kifungo chao sasa kimekamilika kwa kuwa tayari walikuwa wametumia muda fulani gerezani kabla ya hukumu kutolewa.

Olga, mke wa Denis, anasema hivi kuhusu kile kilichowasaidia yeye na Denis walipokuwa wametenganishwa: “Tuliandikiana barua, na katika barua hizo, tulitiana moyo kupitia maandiko. Andiko moja ambalo lilitusaidia sana ni Mhubiri 8:12, ambapo Sulemani aliandika: ‘Ninajua kwamba mambo yatawaendea vema wale wanaomwogopa Mungu wa kweli.’ Mstari huo ulitusaidia kuwa na uhakika kwamba ikiwa tutaendelea kumtumikia Yehova bila kukata tamaa, atatupatia nguvu za kuendelea kuvumilia.”

Kesi yake iliposikilizwa kwa mara ya mwisho mahakamani, Aleksandr alilinganisha hali yake na hali ya nabii Danieli. Aleksandr anasema: “Ingawa alikabili hatari ya kuuawa, imani ya Danieli ilimchochea kuendelea kusali kwa Yehova Mungu. Nitaendelea kumwomba Mungu anipe imani kama hiyo, ambayo haiwezi kupotea kwa sababu ya mateso.”

Tunashangilia pamoja na Denis na Aleksandr kwa kuungana tena na familia zao. Mambo ambayo wamekabili yanatuthibitishia ukweli wa ahadi inayopatikana kwenye Zaburi 4:3 inayosema: “Jueni kwamba Yehova atamtendea mshikamanifu wake kwa njia ya pekee; Yehova atasikia [tunapomlilia].”