Hamia kwenye habari

FEBRUARI 10, 2021
URUSI

Ndugu Dennis Christensen Anyimwa Msamaha

Ndugu Dennis Christensen Anyimwa Msamaha

Februari 10, 2021, Mahakama ya Eneo la Kursk ilikataa ombi la Ndugu Dennis Christensen la kuachiliwa mapema. Alikuwa ameiomba mahakama ibadili sehemu iliyobaki ya kifungo chake na faini. Kwa zaidi ya mwaka mmoja, Dennis amestahili kuachiliwa mapema, hata hivyo, maombi yake yanaendelea kukataliwa.

Hivi karibuni, Dennis alimwandikia barua mke wake, Irina. Alimwandikia mojawapo ya Maandiko anayopenda zaidi: “Basi tusife moyo katika kufanya mema, kwa maana kwa wakati unaofaa tutavuna ikiwa hatutachoka kabisa.” (Wagalatia 6:9) Aliandika kuhusu uhakika wake kwamba Yehova atawathawabisha ikiwa wataendelea kutenda mema, kuwasaidia wengine, na ikiwa hawatakufa moyo. Pia alisema kwamba angependa kutoka gerezani akiwa mwenye nguvu zaidi kiroho kuliko wakati ambapo kifungo chake kilianza.

Dennis amekuwa gerezani mbali na Irina tangu Mei 2017—karibu miaka minne. Dennis na Irina wanaendelea kutuwekea mfano mzuri kwa kumtegemea Yehova, kudumisha amani ya moyoni, na kuendelea kudumisha ushikamanifu usioyumbishwa.—Wafilipi 1:14.