SEPTEMBA 27, 2023
URUSI
Ndugu Nikolay Voishchev Ahukumiwa Kifungo cha Miaka Mitatu Gerezani
Septemba 14, 2023, Mahakama ya Jiji la Maykop iliyo katika Jamhuri ya Adygeya ilimhukumu Ndugu Nikolay Voishchev kifungo cha miaka mitatu gerezani. Amekuwa mahabusu tangu Oktoba 20, 2022, na ataendelea kubaki gerezani.
Maelezo Mafupi Kumhusu
Tunasikitishwa sana kusikia kwamba Nikolay atafungwa gerezani, hata hivyo, tuna uhakika kwamba Yehova ataendelea kumfariji na kumpa nguvu, pamoja na ndugu na dada zetu wote wanaokabili majaribu.—Zaburi 119:76.
Mfuatano wa Matukio
Oktoba 19, 2022
Kesi ya uhalifu yafunguliwa
Oktoba 20, 2022
Nyumba yake ilifanyiwa msako. Nikolay alihojiwa na kuwekwa kizuizini
Oktoba 21, 2022
Alihamishiwa mahabusu
Januari 11, 2023
Hakimu aliombwa amruhusu Nikolay kutumikia kifungo cha nyumbani badala ya kuwa mahabusu kwa sababu ya matatizo ya kiafya. Hakimu alikataa ombi hilo na badala yake akamwongezea Nikolay muda wa kukaa mahabusu
Januari 25, 2023
Kesi ya uhalifu ilianza
Septemba 14, 2023
Alihukumiwa kifungo cha miaka mitatu gerezani
a Kwa kuwa Ndugu Voishchev alikuwa mahabusu, hatukuweza kupata maelezo kutoka kwake.