Hamia kwenye habari

Ndugu Moskalenko, nje ya mahakama baada ya kuachiliwa kutoka gerezani

SEPTEMBA 4, 2019
URUSI

Ndugu Valeriy Moskalenko Aachiliwa Kutoka Gerezani

Ndugu Valeriy Moskalenko Aachiliwa Kutoka Gerezani

Mnamo Septemba 2, 2019, Mahakama ya Wilaya ya Zheleznodorozhniy, nchini Urusi, ilimhukumu Ndugu Valeriy Moskalenko atumikie kwa miaka miwili na miezi miwili katika utumishi wa kijamii na kuzuiliwa kwa miezi mingine sita. Hatalazimika kuendelea kukaa gerezani.

Baada ya uamuzi huo kutolewa, Ndugu Moskalenko aliwekwa huru kutoka kizuizini na kushangiliwa na familia na marafiki zake. Amekuwa mahabusu tangu Agosti 2, 2018. Kabla ya kukamatwa, alifanya kazi ya msaidizi wa kondakta wa garimoshi huku akimtunza mama yake aliyekuwa mgonjwa. Katika muda ambao atakuwa amezuiliwa, hataruhusiwa kusafiri nje ya eneo la Khabarovsk na kila mwezi atalazimika kuripoti kwa maofisa wa masuala ya wahalifu.

Katika maneno yake ya mwisho mahakamani mnamo Agosti 30, Ndugu Moskalenko alisema hivi: “Siwezi kamwe kuwazia kutenda kinyume na mapenzi ya Mungu ambayo yameandikwa waziwazi katika Biblia. Na hata nikishinikizwa au kuadhibiwa kadiri gani, hata nihukumiwe kifo, ninasema kwamba sitamkana kamwe Muumba mweza-yote wa ulimwengu, Yehova Mungu.”

Yaroslav Sivulskiy, mwakilishi wa Shirika la Ulaya la Mashahidi wa Yehova, alisema: “Ingawa hatukubaliani na uamuzi uliosema ana hatia, tunafurahi kwamba Valeriy anaweza kurudi nyumbani.”

Zaidi ya Ndugu Moskalenko, ndugu zetu wengine saba katika eneo la Khabarovsk wanasubiri uamuzi katika kesi zao za uhalifu.

Tunamshukuru Yehova kwamba Ndugu Moskalenko alidumisha imani yake ikiwa thabiti alipokuwa kizuizini. Tunasali kwamba Yehova ataendelea kuwapa nguvu ndugu na dada zetu wote wanaovumilia mateso kwa sababu ya imani yao inayotegemea Biblia.—Isaya 40:31.