Hamia kwenye habari

Ndugu na dada walio na umri wa zaidi ya miaka 60 nchini Urusi ambao wamehukumiwa kuwa wahalifu kwa sababu ya imani yao

AGOSTI 2, 2021
URUSI

Ndugu Waaminifu Wenye Umri Mkubwa Wadumisha Shangwe Licha ya Mateso

Ndugu Waaminifu Wenye Umri Mkubwa Wadumisha Shangwe Licha ya Mateso

Tangu marufuku ilipotangazwa dhidi ya mashirika ya Mashahidi wa Yehova nchini Urusi, wenye mamlaka wamewatesa ndugu na dada nchini kote—kuanzia wenye umri wa miaka 18 hadi wenye umri mkubwa wa miaka 89. Kufikia Julai 2021, ndugu na dada 18 wenye umri wa miaka 60 au zaidi wamehukumiwa kwa sababu tu ya kuabudu kwa amani. Watatu kati yao sasa wako gerezani. a Ripoti ya 4 ya Baraza Linaloongoza ya 2021 ilikazia mashambulizi yenye kuchukiza dhidi ya ndugu na dada zetu wenye umri mkubwa.

Ndugu na dada zetu wenye umri mkubwa wamefauluje kuvumilia mateso hayo? Tunafurahi kushiriki pamoja nanyi maelezo ya baadhi ya waamini wenzetu ambao wamedumisha uaminifu.

Tunashukuru sana kwa mfano bora ambao ndugu hao waaminifu wenye umri mkubwa nchini Urusi wanatuwekea. Msimamo wao wenye ujasiri wa kutetea uadilifu unastahili kuigwa, na muhimu zaidi ni maridadi machoni pa Mungu.—Methali 16:31.

a Dada Valentina Baranovskaya, mwenye umri wa miaka 70, anatumikia kifungo cha miaka miwili gerezani. Ndugu Aleksandr Ivshin, mwenye umri wa miaka 63, anatumikia kifungo cha miaka saba na nusu gerezani. Na Ndugu Yuriy Savelyev, mwenye umri wa miaka 68, anatumikia kifungo cha miaka sita gerezani.