JANUARI 27, 2022
URUSI
Ndugu Wawili Wauona Mkono wa Yehova na Kuendelea Kuwa Jasiri
Mahakama ya Wilaya ya Kirsanovskiy katika Eneo la Tambov itatangaza uamuzi wake hivi karibuni katika kesi inayowahusu Ndugu Anton Kuzhelkov na Nikolay Prokhorov. Mwendesha-mashtaka bado hajatoa hukumu anayopendekeza.
Mfuatano wa Matukio
Desemba 21, 2020
Kesi ya uhalifu ilifunguliwa dhidi ya Anton na Nikolay kwa sababu ya kupanga utendaji wa shirika lenye msimamo mkali
Desemba 24, 2020
Wapelelezi walifanya upekuzi katika maeneo 19 kutia ndani nyumba ya Anton. Alipelekwa eneo lililo umbali wa kilomita 350 kutoka nyumbani kwake ili kuhojiwa. Nikolay alihojiwa kisha akaamriwa asiondoke katika eneo hilo
Desemba 25, 2020
Anton hakuruhusiwa kurudi nyumbani, alipelekwa mahabusu
Agosti 30, 2021
Anton alihamishwa na kuzuiliwa kwenye kituo kingine
Maelezo Mafupi Kuwahusu
Tuna uhakika kwamba Yehova ataendelea kuwapa ujasiri na kuwategemeza ndugu na dada zetu wanaokabili mateso.—Methali 1:33.
a Ndugu Kuzhelkov kwa sasa yuko mahabusu. Haikuwezekana kuzungumza naye.