Hamia kwenye habari

FEBRUARI 12, 2020
URUSI

Ndugu Yevgeniy Aksenov Ameshtakiwa kwa Kuzungumzia Kanuni za Biblia

Ndugu Yevgeniy Aksenov Ameshtakiwa kwa Kuzungumzia Kanuni za Biblia

Ijumaa, Februari 14, 2020, Mahakama ya Wilaya ya Zheleznodorozhniy huko Khabarovsk, itatangaza uamuzi wake katika kesi inayomhusu Ndugu Yevgeniy Aksenov. Mwendesha mashtaka ameomba ahukumiwe kifungo cha miaka mitatu gerezani.

Aprili 21, 2018, Ndugu Aksenov alikutana na marafiki na watu wengine alioshirikiana nao katika ukumbi wa mikutano katika hoteli fulani ili kuzungumzia Biblia. Alizungumza nao kuhusu jinsi kanuni za Biblia zinavyoweza kuimarisha familia zao. Kwa sababu hiyo alituhumiwa kuwa “mhalifu aliye hatari kwa jamii” na kuhukumiwa kwa kosa la “kupanga shughuli za tengenezo lenye msimamo mkali.” Kesi yake ilianza kusikilizwa Oktoba 21, 2019.

Kesi ya Ndugu Aksenov inapokaribia kumalizika, tunasali kwamba yeye na familia yake wataendelea kumtegemea Yehova, wakiamini kabisa ahadi yake iliyoongozwa na roho kwamba washikamanifu wake “hawakosi chochote.”—Zaburi 34:9.