Hamia kwenye habari

Ndugu Yuriy Savelyev baada ya kuachiliwa kutoka gerezani

JULAI 20, 2023
URUSI

Ndugu Yuriy Savelyev Aachiliwa Huru

Ndugu Yuriy Savelyev Aachiliwa Huru

Julai 19, 2023, Ndugu Yuriy Savelyev aliachiliwa kutoka gerezani mjini Rubtsovsk. Aliwekwa kizuizini tangu Novemba 9, 2018, na amekaa gerezani kwa zaidi ya miaka minne na nusu.

Yuriy alipata matatizo ya afya akiwa gerezani kwa sababu ya mazingira yasiyo safi. Isitoshe, mara kadhaa aliwekwa kwenye vyumba vya adhabu gerezani kwa msingi wa ripoti zisizo za kweli. Licha ya hali hizo ngumu, Yuriy alidumisha mtazamo wake mzuri kwa kutegemea nguvu alizopata kwa sababu ya kusali kwa Yehova. Kwa kuwa Yuriy alikuwa mwenye fadhili na alionyesha sifa za Kikristo, wengi kati ya wafungwa wenzake na walinzi wa gereza walimheshimu.

Kikundi cha ndugu na dada wakimkaribisha Yuriy nje ya gereza

Muda mfupi kabla ya hukumu kutolewa dhidi yake, Yuriy alizungumza na mahakama na kunukuu Mathayo 22:37 ambapo Yesu alisema: “Lazima umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote.” Yuriy ameweka mfano mzuri kwa sababu ameishi kupatana na maneno hayo na amedumisha utimilifu wake kwa Yehova. Tunajua kwamba Yehova ataendelea kumbariki Yuriy kwa kuwa ameonyesha imani, upendo, na uvumilivu.