Hamia kwenye habari

Ndugu Yuriy Zalipayev akitoa maelezo yake ya kumalizia mahakamani

OKTOBA 7, 2020
URUSI

Ndugu Yuriy Zalipayev Ametangazwa Kuwa Hana Hatia!

Ndugu Yuriy Zalipayev Ametangazwa Kuwa Hana Hatia!

Oktoba 7, 2020, Mahakama ya Wilaya ya Mayskiy katika Jamhuri ya Kabardino-Balkaria ilitangaza kwamba Ndugu Yuriy Zalipayev hana hatia na ikamwondolea mashtaka yote. Mwendesha-mashtaka ana siku kumi za kukata rufaa.

Mwendesha-mashtaka alidai kwamba Ndugu Zalipayev alikuwa na hatia ya kuwachochea wengine kutenda kwa jeuri. Hata hivyo, zaidi ya watu 30 walitoa ushahidi kwamba alichofanya tu ni kuwatia moyo wengine wasome Biblia na kuwaonyesha watu wengine upendo na fadhili.

Uamuzi huo wa mahakama kwamba “hana hatia” unategemea pia mkataa wa karibuni uliofikiwa na Kamati ya Umoja wa Mataifa ya Vifungo Visivyo vya Haki uliothibitisha kwamba Mashahidi wa Yehova hawatendi wala kuchochea jeuri katika njia yoyote ile.

Baada ya uamuzi huo kutangazwa, Ndugu Zalipayev alisema hivi: “Watu wa familia yangu pamoja na marafiki walikuwa wamejitayarisha kupokea uamuzi usiofaa. Namshukuru Yehova kwamba sikuwa na mkazo wakati wa kesi. Nina furaha sana na ninawashukuru wote walionitetea kwamba sina hatia.”