JULAI 8, 2024
URUSI
‘Ninajionea Baraka Maishani Mwangu’
Mahakama ya Wilaya ya Vyselkovskiy iliyo katika Eneo la Krasnodar itatangaza uamuzi wake hivi karibuni katika kesi inayomhusu Ndugu Viktor Spirichev. Mwendesha mashtaka bado hajatoa ombi la hukumu anayopendekeza.
Maelezo Mafupi Kumhusu
Tunafurahi kujua kwamba tunaweza kutumaini fadhili zisizostahiliwa za Yehova tunapoendelea ‘kutendeana kwa unyenyekevu.’—1 Petro 5:5.
Mfuatano wa Matukio
Februari 13, 2022
Wenye mamlaka walifanya msako kwenye nyumba 25 hivi za Mashahidi wa Yehova katika eneo la Vyselki na Berezanskaya, kutia ndani nyumba ya Viktor na Larisa
Mei 23, 2023
Kesi ya uhalifu ilifunguliwa. Alishtakiwa kwa kushiriki utendaji wa shirika lenye msimamo mkali. Akaunti zake za benki zilifungwa
Julai 11, 2023
Alihojiwa na wenye mamlaka
Julai 22, 2023
Alihojiwa kwa mara ya pili. Akawekewa vizuizi vya kusafiri
Januari 30, 2024
Kesi ya uhalifu ilianza