Hamia kwenye habari

Ndugu Viktor Spirichev

JULAI 8, 2024
URUSI

‘Ninajionea Baraka Maishani Mwangu’

‘Ninajionea Baraka Maishani Mwangu’

Mahakama ya Wilaya ya Vyselkovskiy iliyo katika Eneo la Krasnodar itatangaza uamuzi wake hivi karibuni katika kesi inayomhusu Ndugu Viktor Spirichev. Mwendesha mashtaka bado hajatoa ombi la hukumu anayopendekeza.

Maelezo Mafupi Kumhusu

Tunafurahi kujua kwamba tunaweza kutumaini fadhili zisizostahiliwa za Yehova tunapoendelea ‘kutendeana kwa unyenyekevu.’​—1 Petro 5:5.

Mfuatano wa Matukio

  1. Februari 13, 2022

    Wenye mamlaka walifanya msako kwenye nyumba 25 hivi za Mashahidi wa Yehova katika eneo la Vyselki na Berezanskaya, kutia ndani nyumba ya Viktor na Larisa

  2. Mei 23, 2023

    Kesi ya uhalifu ilifunguliwa. Alishtakiwa kwa kushiriki utendaji wa shirika lenye msimamo mkali. Akaunti zake za benki zilifungwa

  3. Julai 11, 2023

    Alihojiwa na wenye mamlaka

  4. Julai 22, 2023

    Alihojiwa kwa mara ya pili. Akawekewa vizuizi vya kusafiri

  5. Januari 30, 2024

    Kesi ya uhalifu ilianza