Hamia kwenye habari

Ndugu Ildar Urazbakhtin

OKTOBA 18, 2022
URUSI

“Ninajivunia Kuitwa kwa Jina la Yehova”

“Ninajivunia Kuitwa kwa Jina la Yehova”

Oktoba 10, 2022, Mahakama ya Wilaya ya Kezhemskiy iliyo katika Eneo la Krasnoyarsk ilimhukumu Ndugu Ildar Urazbakhtin. Alihukumiwa kifungo cha nje cha miaka mitatu na hahitaji kwenda gerezani wakati huu.

Mfuatano wa Matukio

  1. Julai 20, 2021

    Nyumba tano hivi za Mashahidi wa Yehova zilifanyiwa msako katika jiji la Kodinsk, kutia ndani nyumba ya Ildar na familia yake. Alikamatwa na kupelekwa mahabusu

  2. Julai 21, 2021

    Aliachiliwa na kuwekwa katika kifungo cha nyumbani. Hakuruhusiwa kutumia simu au Intaneti

  3. Septemba 20, 2021

    Aliachiliwa kutoka katika kifungo cha nyumbani na akawekewa vizuizi vya kusafiri

  4. Januari 13, 2022

    Alishtakiwa kwa kufanya mikutano kupitia mtandao ambapo “aliwatia moyo ndugu na dada kusoma Biblia kwa kina na kusaidiana”

  5. Machi 30, 2022

    Kesi ya uhalifu ilianza

Maelezo Mafupi Kumhusu

Mambo ambayo Ildar pamoja na ndugu na dada wengine wanapitia nchini Urusi yanatukumbusha kwamba Mungu wetu Yehova, anatamani sana na yuko tayari kutusaidia katika “nyakati za taabu.”​—Zaburi 46:1.