AGOSTI 10, 2023
URUSI
Wameazimia Kuwa na Shangwe Licha ya Mateso
Mahakama ya Jiji la Syktyvkarskiy iliyo katika Jamhuri ya Komi itatangaza hivi karibuni uamuzi wake katika kesi inayowahusu Ndugu Aleksandr Ketov, Ndugu Andrey Kharlamov, Ndugu Aleksandr Kruglyakov, Dada Lidiya Nekrasova, na Ndugu Sergey Ushakhin. Mwendesha-mashtaka bado hajatoa ombi la hukumu anayopendekeza.
Maelezo Mafupi Kuwahusu
Kama tulivyoona kwenye masimulizi haya Yehova huwapa ndugu na dada zetu “uwezo kamili” ili waweze kuvumilia majaribu na kubaki waaminifu.— Isaya 40:29.
Mfuatano wa Matukio
Machi 2, 2021
Nyumba 14 za Mashahidi wa Yehova zilifanyiwa msako jijini Syktyvkar. Aleksandr Ketov, Andrey Kharlamov, na Aleksandr Kruglyakov walipelekwa kizuizini. Lidiya Nekrasova na Sergey Ushakhin waliwekewa vizuizi vya kusafiri
Machi 3, 2021
Aleksandr Ketov na Andrey Kharlamov waliachiliwa kutoka kizuizini na kuwekwa chini ya kifungo cha nyumbani. Aleksandr Kruglyakov alipelekwa mahabusu
Aprili 27, 2021
Andrey Kharlamov aondolewa kifungo cha nyumbani
Aprili 28, 2021
Aleksandr Ketov aondolewa kifungo cha nyumbani, na Aleksandr Kruglyakov aachiliwa kutoka mahabusu
Aprili 19, 2022
Kesi ya uhalifu yaanza
Juni 9, 2022
Hakimu alisema kesi hiyo haina ushahidi wa kutosha na akairudisha kwa mwendesha-mashtaka
Februari 14, 2023
Kesi hiyo yaanza kusikilizwa tena na hakimu mwingine