FEBRUARI 13, 2024
URUSI
Wanakazia Fikira Heshima ya Kumtumikia Yehova
Mahakama ya Wilaya ya Vyselkovskiy iliyo katika Eneo la Krasnodar itatangaza uamuzi wake hivi karibuni katika kesi inayowahusu Ndugu Yevgeniy Bochko, Ndugu Vladimir Kolesnikov, Ndugu Aleksey Shubnikov, Ndugu Vitaliy Ushakov, na Ndugu Valeriy Vechkayev. Mwendesha-mashtaka bado hajatoa ombi la hukumu anayopendekeza.
Maelezo Mafupi Kuwahusu
Tuna uhakika kwamba Yehova ataendelea kuwapa nguvu na shangwe ndugu hao na wale wote wanaoendelea kumtegemea ili kupata msaada.—Zaburi 141:8.
Mfuatano wa Matukio
Februari 11, 2022
Kesi ya uhalifu ilifunguliwa dhidi ya Yevgeniy, Aleksey, Vitaliy, na Valeriy
Februari 13, 2022
Nyumba zilifanyiwa msako. Yevgeniy, Aleksey, na Vitaliy walihojiwa. Vitaliy aliwekwa kizuizini
Februari 15, 2022
Vitaliy alipelekwa mahabusu
Februari 16, 2022
Yevgeniy na Aleksey waliwekewa vizuizi vya kusafiri
Februari 18, 2022
Valeriy aliwekewa vizuizi vya kusafiri
Februari 21, 2022
Kesi ya uhalifu ilianzishwa dhidi ya Vladimir
Machi 15, 2022
Vladimir aliwekewa vizuizi vya kusafiri. Kesi za uhalifu ziliunganishwa na kuwa kesi moja
Septemba 8, 2022
Vitaliy aliachiliwa kutoka mahabusu na kuwekwa katika kifungo cha nyumbani
Oktoba 10, 2022
Vitaliy aliachiliwa kutoka katika kifungo cha nyumbani na kuwekewa vizuizi vya kusafiri
Mei 31, 2023
Kesi ya uhalifu ilianza