Hamia kwenye habari

FEBRUARI 10, 2021
URUSI

Wenye Mamlaka Urusi Wavamia Nyumba 15 Hivi za Mashahidi Katika Jijini la Moscow

Wenye Mamlaka Urusi Wavamia Nyumba 15 Hivi za Mashahidi Katika Jijini la Moscow

Asubuhi ya Februari 10, 2021, wenye mamlaka nchini Urusi walivamia nyumba 15 hivi za ndugu na dada zetu katika jiji la Moscow na maeneo karibu na jiji hilo. Polisi wa eneo hilo na wa kitaifa walishirikiana na maofisa wa Idara ya Usalama wa Taifa (FSB) kufanya msako huo. Maofisa hao waliwakamata ndugu kadhaa ili kuwahoji. Ndugu watatu hivi wamewekwa kizuizini.

Tunaendelea kusali kwa ajili ya ndugu na dada zetu nchini Urusi, tukiwa na uhakika kwamba Yehova atawapa nguvu za kuvumilia mateso hayo.—1 Petro 5:10.