AGOSTI 8, 2024
URUSI
‘Yehova Ni Kimbilio Langu na Mlinzi Wangu’
Mahakama ya Wilaya ya Vyselkovskiy katika Eneo la Krasnodar itatangaza hivi karibuni uamuzi wake katika kesi inayomhusu Dada Lyudmila Zinina. Bado mwendesha-mashtaka hajatoa ombi la hukumu anayopendekeza.
Maelezo Mafupi Kumhusu
Kama Lyudmila, sisi pia na tusitawishe imani yenye nguvu katika Mungu wetu, Yehova, ambaye hawaachi kamwe wale wanaomtumaini.—Kumbukumbu la Torati 31:6.
Mfuatano wa Wakati
Februari 13, 2022
Nyumba ambayo Lyudmila, mume wake, na binti yao Irina wanaishi ilifanyiwa upekuzi
Mei 23, 2023
Kesi ya uhalifu ilifunguliwa. Alishtakiwa kwa kushiriki katika utendaji wa shirika lenye msimamo mkali na kuzungumza kuhusu imani yake
Juni 9, 2023
Jina lake liliongezwa kwenye orodha ya watu wenye msimamo mkali nchini Urusi
Julai 11, 2023
Aliwekewa vizuizi vya kusafiri
Februari 8, 2024
Kesi ya uhalifu ilianza kusikilizwa