Hamia kwenye habari

NOVEMBA 23, 2017
URUSI

Mahakama ya Urusi Itasikiliza Rufaa ya Kupinga Kutangazwa kwa Biblia Kuwa na “Msimamo Mkali”

Mahakama ya Urusi Itasikiliza Rufaa ya Kupinga Kutangazwa kwa Biblia Kuwa na “Msimamo Mkali”

Desemba 6, 2017, Mahakama ya Mkoa ya Leningrad itasikiliza rufaa ya Mashahidi ya kupinga uamuzi wa mahakama ya chini wa kupiga marufuku Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya katika Kirusi.

Mnamo Agosti 2017, Mahakama ya Jiji la Vyborg ilikubali madai ya mwendesha mashtaka kwamba Tafsiri ya Ulimwengu Mpya si Biblia kwa sababu inataja jina la kibinafsi la Mungu, “Yehova” ambalo limetokana na Tetragramatoni. Madai haya ya mwendesha mashtaka yalifanya akiuke Sheria ya Kupambana na Shughuli Zenye Msimamo Mkali, ambayo inakataza kutangaza vitabu vitakatifu kuwa na msimamo mkali.

Mashahidi wa Yehova ambao ni wachapishaji wa Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Kirusi, wamesikitishwa sana na uamuzi wa Mahakama ya Jiji la Vyborg wa kutangaza Biblia kuwa chapisho “lenye msimamo mkali.” Tafsiri ya Ulimwengu Mpya imechapishwa ikiwa nzima au kwa sehemu katika lugha 161 na ni tafsiri inayoheshimiwa, sahihi, na rahisi kuisoma. Zaidi ya nakala milioni 200 zimegawanywa.