Hamia kwenye habari

JULAI 4, 2014
URUSI

Mashahidi wa Yehova Washtakiwa Jijini Taganrog

Mashahidi wa Yehova Washtakiwa Jijini Taganrog

Kufikia Julai 2014, kesi ya uhalifu dhidi ya Mashahidi 16 wa Yehova jijini Taganrog, Urusi, haijakamilika, ingawa miezi 14 imepita tangu ilipoanza. Kesi hiyo ilipokuwa ikisikilizwa, mahakama ilichunguza mabuku zaidi ya 60 yaliyokuwa na ule unaodaiwa kuwa ushahidi uliotia ndani programu za ibada zilizorekodiwa, sala, na usomaji wa Biblia​—mambo yaleyale yanayofanywa katika ibada za Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote.

Uhuru wa ibada wa washtakiwa hao pamoja na Mashahidi wengine 800 jijini Taganrog umo hatarini. Mashahidi wote 16 wamesema wazi kwamba hawatakana imani yao na wataendelea kuabudu wakiwa Mashahidi wa Yehova haidhuru matokeo ya uamuzi huo yatakuwaje.

Video hii inaonyesha jinsi baadhi ya washtakiwa na mawakili wao wanavyopambana ili kudumisha uhuru wao wenye thamani wa kuabudu licha ya kushtakiwa kama wahalifu.