Hamia kwenye habari

Kibanda cha jw.org kwenye Maonyesho ya Kimataifa ya Zimbabwe chavutia wageni wengi

JUNI 13, 2023
ZIMBABWE

Kuwafikia Watu Mbalimbali Kwenye Maonyesho ya Kimataifa ya Zimbabwe ya 2023

Kuwafikia Watu Mbalimbali Kwenye Maonyesho ya Kimataifa ya Zimbabwe ya 2023

Maonyesho ya Kimataifa ya Zimbabwe (ZITF) yalifanywa kuanzia Aprili 25 hadi 29, 2023, jijini Bulawayo, Zimbabwe. Maonyesho ya ZITF ni mojawapo ya maonyesho makubwa nchini humo na yalikuwa na makampuni 500 kutoka nchi 22 yaliyoonyesha bidhaa zao. Maonyesho hayo yalihudhuriwa na zaidi ya watu 60,000. Mashahidi wa Yehova walishiriki katika maonyesho hayo chini ya kitengo cha elimu.

Kibanda hicho kilikuwa na machapisho ya Biblia katika lugha kumi kutia ndani Lugha ya Ishara ya Zimbabwe kusudi likiwa kuwafikia wageni waliotoka nchi mbalimbali. Wale waliopendezwa walielezwa kuhusu mpango wetu wa kujifunza Biblia pamoja na mwalimu. Kufikia mwisho wa maonyesho hayo, zaidi ya machapisho 12,000 yalikuwa yametolewa na zaidi ya watu 450 walikuwa wameomba kutembelewa na Mashahidi wa Yehova. Dada Eucebiah Mukura, aliyekuwa akiwapokea wageni kwenye kibanda alisema hivi: “Wengi walikubali kujifunza Biblia. Nilifurahi sana kusikia watu wengi wakisema wanatazamia kwa hamu kutembelewa na Mashahidi wa Yehova.”

Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ilikuwepo kwenye kibanda chetu pia. Mwanamke mmoja aliposikia mtu akisoma kwa sauti kubwa tafsiri hiyo kwenye lugha ya Ndebele, alivutiwa na jinsi Biblia hiyo inavyoeleweka kwa urahisi na akaomba apate nakala. Akiwa amesisimka sana mwanamke mwingine alimwonyesha dada yetu programu ya JW Library aliyokuwa amepakua kwenye simu. Mwanamke huyo alisema kwamba alikuwa amepakua programu hiyo ili awe na Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.

Dada Gillian Ellerman ambaye alikuwa akiwahudumia wageni alisema, “Tulifurahia sana maonyesho hayo. Kibanda chetu hakikukauka watu. Bila shaka hilo lilimletea Yehova sifa kwa njia kubwa!”

Tunatiwa moyo sana tunapoona jinsi ndugu na dada zetu nchini Zimbabwe wanavyotumia kila fursa kushiriki na wengine “ujuzi sahihi wa kweli.”​—1 Timotheo 2:4.