Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati 11:1-47

  • Daudi atiwa mafuta na Waisraeli wote kuwa mfalme (1-3)

  • Daudi ateka jiji la Sayuni (4-9)

  • Mashujaa hodari wa Daudi (10-47)

11  Baada ya muda Waisraeli wote wakakusanyika kwa Daudi kule Hebroni+ na kusema: “Tazama! Sisi ni mfupa wako na nyama yako.*+  Zamani, Sauli alipokuwa mfalme, ni wewe uliyewaongoza Waisraeli vitani.*+ Na Yehova Mungu wako alikuambia hivi: ‘Utawachunga watu wangu Waisraeli, nawe utakuwa kiongozi wa watu wangu Waisraeli.’”+  Basi wazee wote wa Israeli wakaja kwa mfalme huko Hebroni, na Daudi akafanya agano nao huko Hebroni mbele za Yehova. Kisha wakamtia mafuta Daudi awe mfalme wa Israeli,+ kulingana na neno la Yehova kupitia Samweli.+  Baadaye Daudi na Waisraeli wote wakaenda Yerusalemu, yaani, Yebusi,+ ambako Wayebusi+ walikuwa wakiishi.  Wakaaji wa Yebusi walimdhihaki Daudi wakisema: “Hutaingia humu kamwe!”+ Hata hivyo, Daudi aliiteka ngome ya Sayuni,+ ambayo sasa ni Jiji la Daudi.+  Kwa hiyo Daudi akasema: “Yeyote atakayekuwa wa kwanza kuwashambulia Wayebusi atakuwa kiongozi* na mkuu.” Basi Yoabu+ mwana wa Seruya akawa wa kwanza kupanda huko kuwashambulia, akawa kiongozi.  Kisha Daudi akaanza kukaa katika ngome hiyo. Ndiyo sababu waliiita Jiji la Daudi.  Akaanza kujenga jiji hilo pande zote, kuanzia kwenye Kilima* mpaka kwenye maeneo yanayozunguka, na Yoabu akajenga upya sehemu zilizobaki za jiji hilo.  Kwa hiyo Daudi akawa mkuu zaidi na zaidi,+ na Yehova wa majeshi alikuwa pamoja naye. 10  Sasa hawa ndio viongozi wa mashujaa hodari wa Daudi, waliomuunga mkono kwa dhati katika utawala wake, pamoja na Waisraeli wote, ili wamweke kuwa mfalme kulingana na neno alilosema Yehova kuhusu Israeli.+ 11  Hii ndiyo orodha ya mashujaa hodari wa Daudi: Yashobeamu+ mwana wa Mhakmoni, kiongozi wa wale watatu.+ Wakati mmoja, alitumia mkuki wake kuwaua watu 300.+ 12  Aliyemfuata ni Eleazari+ mwana wa Dodo mwana wa Ahohi.+ Alikuwa miongoni mwa mashujaa hao watatu hodari. 13  Alikuwa na Daudi kule Pas-damimu,+ ambako Wafilisti walikuwa wamekusanyika kwa ajili ya vita. Basi palikuwa na shamba lililojaa shayiri, na watu walikuwa wamekimbia kwa sababu ya Wafilisti. 14  Lakini alisimama katikati ya shamba hilo na kuwazuia Wafilisti wasiingie humo, naye aliendelea kuwaua Wafilisti, hivi kwamba Yehova akawapa ushindi* mkubwa.+ 15  Viongozi watatu kati ya wale viongozi 30 walishuka mwambani kwa Daudi, katika pango la Adulamu,+ wakati jeshi la Wafilisti lilipokuwa limepiga kambi katika Bonde la* Refaimu.+ 16  Wakati huo Daudi alikuwa ndani ya ngome, na kikosi cha wanajeshi Wafilisti kilikuwa Bethlehemu. 17  Kisha Daudi akasema alichotamani: “Laiti ningekunywa maji kutoka katika tangi lililo karibu na lango la Bethlehemu!”+ 18  Ndipo wale mashujaa watatu wakaingia kwa nguvu katika kambi ya Wafilisti, wakateka maji kutoka katika tangi hilo lililo karibu na lango la Bethlehemu na kumletea Daudi; lakini Daudi akakataa kuyanywa, akayamwaga mbele za Yehova. 19  Akasema: “Ni jambo nisiloweza kamwe kuwazia, kulingana na maoni ya Mungu wangu, kufanya hivyo! Je, ninywe damu ya wanaume hawa waliohatarisha uhai wao?”*+ Kwa maana walihatarisha uhai wao kwenda kuyaleta. Basi akakataa kuyanywa. Hayo ndiyo mambo waliyotenda mashujaa wake watatu hodari. 20  Abishai+ ndugu ya Yoabu+ akawa kiongozi wa wengine watatu; alitumia mkuki wake kuwaua watu 300, naye alikuwa maarufu kama wale watatu.+ 21  Ingawa alikuwa mashuhuri zaidi kuliko wale wengine watatu, na alikuwa kiongozi wao, hakuwa shujaa kama wale watatu wa kwanza. 22  Benaya+ mwana wa Yehoyada alikuwa mwanamume jasiri* aliyefanya mambo mengi ya kishujaa kule Kabzeeli.+ Aliwaua wana wawili wa Arieli wa Moabu, naye aliingia ndani ya shimo la maji siku ya theluji na kumuua simba.+ 23  Alimuua pia mwanamume Mmisri aliyekuwa mkubwa isivyo kawaida—mwenye urefu wa mikono mitano.*+ Ingawa Mmisri huyo alikuwa na mkuki mkononi kama mti wa wafumaji wa nguo,+ Benaya alikabiliana naye akiwa na fimbo, akamnyang’anya Mmisri huyo mkuki kutoka mkononi mwake na kumuua kwa mkuki wake mwenyewe.+ 24  Benaya mwana wa Yehoyada alifanya mambo hayo, naye alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu hodari. 25  Ingawa alikuwa mashuhuri hata kuliko wale 30, hakuwa shujaa kama wale watatu.+ Lakini Daudi alimweka kuwa kiongozi wa walinzi wake binafsi. 26  Mashujaa hodari jeshini walikuwa Asaheli+ ndugu ya Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo wa Bethlehemu,+ 27  Shamothi Mharori, Helezi Mpeloni, 28  Ira+ mwana wa Ikeshi Mtekoa, Abiezeri+ Mwanathothi, 29  Sibekai+ Mhusha, Ilai Mwahohi, 30  Maharai+ Mnetofa, Heledi+ mwana wa Baana Mnetofa, 31  Ithai mwana wa Ribai wa jiji la Gibea la Wabenjamini,+ Benaya Mpirathoni, 32  Hurai kutoka katika makorongo* ya Gaashi,+ Abieli Mwarbathi, 33  Azmavethi Mbaharumu, Eliaba Mshaalboni, 34  wana wa Hashemu Mgizoni, Yonathani mwana wa Shagee Mharari, 35  Ahiamu mwana wa Sakari Mharari, Elifali mwana wa Uru, 36  Heferi Mmekerathi, Ahiya Mpeloni, 37  Hezro Mkarmeli, Naarai mwana wa Ezbai, 38  Yoeli ndugu ya Nathani, Mibhari mwana wa Hagri, 39  Seleki Mwamoni, Naharai Mberothi, aliyembebea silaha Yoabu mwana wa Seruya; 40  Ira Mwithri, Garebu Mwithri, 41  Uria+ Mhiti, Zabadi mwana wa Alai, 42  Adina mwana wa Shiza Mrubeni, kiongozi wa Warubeni, aliyekuwa na watu 30; 43  Hanani mwana wa Maaka, Yoshafati Mmithini, 44  Uziya Mwashtarothi, Shama na Yeieli, wana wa Hothamu Mwaroeri; 45  Yediaeli mwana wa Shimri, na Yoha ndugu yake, Mtisi; 46  Elieli Mmahawi, Yeribai na Yoshavia wana wa Elnaamu, na Ithma Mmoabu; 47  Elieli, Obedi, na Yaasieli Mmesoba.

Maelezo ya Chini

Tnn., “Tuna uhusiano wa damu nawe.”
Tnn., “uliyekuwa ukiwatoa nje na kuwaingiza ndani Waisraeli.”
Tnn., “kichwa.”
Au “Milo.” Neno la Kiebrania linalomaanisha “jaza.”
Au “wokovu.”
Au “Nchi Tambarare ya Chini ya.”
Au “nafsi zao.”
Tnn., “mwana wa mwanamume jasiri.”
Urefu wake ulikuwa karibu mita 2.23 (futi 7.3). Angalia Nyongeza B14.
Angalia Kamusi.