Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati 13:1-14

  • Sanduku la agano laletwa kutoka Kiriath-yearimu (1-14)

13  Daudi alishauriana na wakuu wa maelfu na wa mamia na kila kiongozi.+  Kisha Daudi akaliambia kutaniko lote la Waisraeli: “Mkiona ni vema na ikiwa ni jambo linalokubalika kwa Yehova Mungu wetu, acheni tutume ujumbe kwa ndugu zetu waliobaki katika maeneo yote ya Israeli na pia kwa makuhani na Walawi katika majiji yao+ yenye malisho waje kuungana nasi.  Na acheni tulirudishe Sanduku+ la Mungu wetu.” Kwa maana hawakuwa wamelitunza katika siku za Sauli.+  Kutaniko lote likakubali kufanya hivyo, kwa maana watu wote waliliona kuwa jambo jema.  Basi Daudi akawakusanya Waisraeli wote, kuanzia mto wa Misri* mpaka Lebo-Hamathi,*+ ili walete Sanduku la Mungu wa kweli kutoka Kiriath-yearimu.+  Daudi na Waisraeli wote wakapanda kwenda Baala,+ mpaka Kiriath-yearimu, jiji la Yuda, ili kuleta kutoka huko Sanduku la Mungu wa kweli, Yehova, anayeketi kwenye kiti cha ufalme juu ya* makerubi,+ mahali ambapo watu husali katika jina lake.  Hata hivyo, walilitoa Sanduku la Mungu wa kweli katika nyumba ya Abinadabu na kuliweka juu ya gari jipya la kukokotwa,+ na Uza na Ahio walikuwa wakiliongoza gari hilo.+  Daudi na Waisraeli wote walikuwa wakisherehekea mbele za Mungu wa kweli kwa nguvu zao zote, kwa nyimbo, vinubi, vinanda vinginevyo, matari,+ matoazi,+ na tarumbeta.+  Lakini walipofika kwenye uwanja wa kupuria wa Kidoni, Uza aliunyoosha mkono wake haraka na kulikamata Sanduku hilo, kwa sababu ng’ombe walikuwa karibu kuliangusha. 10  Ndipo hasira ya Yehova ikawaka dhidi ya Uza, Naye akamuua kwa sababu aliunyoosha mkono wake na kulikamata Sanduku+ hilo, naye akafa hapo mbele za Mungu.+ 11  Lakini Daudi akakasirika kwa sababu hasira kali ya Yehova iliwaka dhidi ya Uza; na tangu siku hiyo mahali hapo panaitwa Peres-uza.* 12  Basi Daudi akamwogopa Mungu wa kweli siku hiyo na kusema: “Ninawezaje kulileta kwangu Sanduku la Mungu wa kweli?”+ 13  Daudi hakulileta Sanduku hilo mahali alipokuwa katika Jiji la Daudi, lakini aliagiza lipelekwe katika nyumba ya Obed-edomu, Mgathi. 14  Sanduku la Mungu wa kweli lilikaa pamoja na watu wa nyumba ya Obed-edomu, likabaki katika nyumba yake kwa miezi mitatu, na Yehova akaendelea kuwabariki watu wa nyumba ya Obed-edomu na vitu vyote alivyokuwa navyo.+

Maelezo ya Chini

Au “kuanzia Shihori huko Misri.”
Au “njia ya kuingia Hamathi.”
Au labda, “katikati ya.”
Maana yake “Ghadhabu Dhidi ya Uza.”