Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati 2:1-55

  • Wana 12 wa Israeli (1, 2)

  • Wazao wa Yuda (3-55)

2  Hawa ndio waliokuwa wana wa Israeli:+ Rubeni,+ Simeoni,+ Lawi,+ Yuda,+ Isakari,+ Zabuloni,+  Dani,+ Yosefu,+ Benjamini,+ Naftali,+ Gadi,+ na Asheri.+  Wana wa Yuda walikuwa Eri, Onani, na Shela. Binti ya Shua, mwanamke Mkanaani, alimzalia wana hao watatu.+ Lakini Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, hakumpendeza Yehova, kwa hiyo Akamuua.+  Tamari,+ binti mkwe wa Yuda, alimzalia Yuda wana walioitwa Perezi+ na Zera. Yuda alikuwa na jumla ya wana watano.  Wana wa Perezi walikuwa Hezroni na Hamuli.+  Wana wa Zera walikuwa Zimri, Ethani, Hemani, Kalkoli, na Dara. Wote walikuwa watano.  Mwana* wa Karmi alikuwa Akari,* aliyewaletea Waisraeli msiba,*+ ambaye alikosa uaminifu kuhusiana na kitu kilichopaswa kuharibiwa.+  Mwana* wa Ethani alikuwa Azaria.  Wana waliozaliwa na Hezroni walikuwa Yerahmeeli,+ Ramu,+ na Kelubai.* 10  Ramu alimzaa Aminadabu.+ Aminadabu akamzaa Nashoni+ mkuu wa wazao wa Yuda. 11  Nashoni akamzaa Salma.+ Salma akamzaa Boazi.+ 12  Boazi akamzaa Obedi. Obedi akamzaa Yese.+ 13  Yese akamzaa mzaliwa wake wa kwanza Eliabu, wa pili Abinadabu,+ wa tatu Shimea,+ 14  wa nne Nethaneli, wa tano Radai, 15  wa sita Ozemu, na wa saba Daudi.+ 16  Dada zao walikuwa Seruya na Abigaili.+ Wana wa Seruya walikuwa Abishai,+ Yoabu,+ na Asaheli,+ wana watatu. 17  Abigaili alimzaa Amasa,+ na baba ya Amasa alikuwa Yetheri, Mwishmaeli. 18  Kalebu* mwana wa Hezroni aliwazaa wana kupitia Azuba mke wake na kupitia Yeriothi; na hawa ndio waliokuwa wana wa Azuba: Yesheri, Shobabu, na Ardoni. 19  Azuba alipokufa, Kalebu alimwoa Efrathi,+ aliyemzalia Kalebu mwana aliyeitwa Huru.+ 20  Huru akamzaa Uri. Uri akamzaa Bezaleli.+ 21  Baadaye Hezroni akalala na binti ya Makiri+ baba ya Gileadi.+ Hezroni alikuwa na umri wa miaka 60 alipomwoa, naye akamzalia Segubu. 22  Segubu akamzaa Yairi,+ aliyekuwa na majiji 23 katika nchi ya Gileadi.+ 23  Baadaye Geshuri+ na Siria+ wakachukua Hawoth-yairi+ kutoka kwao, pamoja na Kenathi+ na miji yake, majiji 60. Wote hao walikuwa wazao wa Makiri baba ya Gileadi. 24  Baada ya Hezroni+ kufa huko Kalebu-efratha, Abiya mke wake alimzalia Hezroni mwana aliyeitwa Ashuri,+ baba ya Tekoa.+ 25  Wana wa Yerahmeeli mzaliwa wa kwanza wa Hezroni walikuwa Ramu mzaliwa wa kwanza, Buna, Oreni, Ozemu, na Ahiya. 26  Yerahmeeli alikuwa na mke mwingine aliyeitwa Atara. Alikuwa mama ya Onamu. 27  Wana wa Ramu mzaliwa wa kwanza wa Yerahmeeli walikuwa Maazi, Yamini, na Ekeri. 28  Wana wa Onamu walikuwa Shamai na Yada. Wana wa Shamai walikuwa Nadabu na Abishuri. 29  Mke wa Abishuri aliitwa Abihaili, alimzalia Abishuri wana walioitwa Abani na Molidi. 30  Wana wa Nadabu walikuwa Seledi na Apaimu. Lakini Seledi alikufa bila watoto.* 31  Mwana* wa Apaimu alikuwa Ishi. Na mwana* wa Ishi alikuwa Sheshani, na mwana* wa Sheshani alikuwa Alai. 32  Wana wa Yada ndugu ya Shamai walikuwa Yetheri na Yonathani. Lakini Yetheri alikufa bila watoto.* 33  Wana wa Yonathani walikuwa Pelethi na Zaza. Hao ndio waliokuwa wazao wa Yerahmeeli. 34  Sheshani hakuwa na watoto wa kiume, alikuwa na mabinti tu. Sheshani alikuwa na mtumishi Mmisri aliyeitwa Yarha. 35  Sheshani akamchukua binti yake na kumpa Yarha mtumishi wake awe mke wake, na binti huyo akamzalia mwana aliyeitwa Atai. 36  Atai akamzaa Nathani. Nathani akamzaa Zabadi. 37  Zabadi akamzaa Eflali. Eflali akamzaa Obedi. 38  Obedi akamzaa Yehu. Yehu akamzaa Azaria. 39  Azaria akamzaa Helezi. Helezi akamzaa Eleasa. 40  Eleasa akamzaa Sismai. Sismai akamzaa Shalumu. 41  Shalumu akamzaa Yekamia. Yekamia akamzaa Elishama. 42  Wana wa Kalebu*+ ndugu ya Yerahmeeli walikuwa Mesha mzaliwa wake wa kwanza, aliyekuwa baba ya Zifu, na wana wa Maresha baba ya Hebroni. 43  Wana wa Hebroni walikuwa Kora, Tapua, Rekemu, na Shema. 44  Shema akamzaa Rahamu baba ya Yorkeamu. Rekemu akamzaa Shamai. 45  Mwana wa Shamai alikuwa Maoni. Maoni alikuwa baba ya Beth-suri.+ 46  Efa suria wa Kalebu alimzaa Harani, Mosa, na Gazezi. Harani akamzaa Gazezi. 47  Wana wa Yahdai walikuwa Regemu, Yothamu, Geshani, Peleti, Efa, na Shaafu. 48  Maaka suria wa Kalebu alimzaa Sheberi na Tirhana. 49  Baada ya muda akamzaa Shaafu baba ya Madmana+ na Sheva baba ya Makbena na Gibea.+ Binti ya Kalebu+ alikuwa Aksa.+ 50  Hao ndio waliokuwa wazao wa Kalebu. Wana wa Huru+ mzaliwa wa kwanza wa Efratha+ walikuwa Shobali baba ya Kiriath-yearimu,+ 51  Salma baba ya Bethlehemu,+ na Harefu baba ya Beth-gaderi. 52  Shobali baba ya Kiriath-yearimu alikuwa na wana hawa: Haroe na nusu ya watu wa Menuhothi. 53  Koo za Kiriath-yearimu zilikuwa Waithri,+ Waputhu, Washumathi, na Wamishra. Wasorathi+ na Waeshtaoli+ walitokana na koo hizo. 54  Wana wa Salma walikuwa Bethlehemu,+ Wanetofa, Atroth-beth-yoabu, na nusu ya Wamanahathi, na Wazori. 55  Koo za waandishi walioishi Yabesi zilikuwa Watirathi, Washimea, na Wasukathi. Hao walikuwa Wakeni+ wazao wa Hamathi baba wa nyumba ya Rekabu.+

Maelezo ya Chini

Au “taabu; aliyesababisha watengwe.”
Maana yake “Mleta Msiba; Anayesababisha Watu Watengwe.” Katika Yos 7:1, anaitwa pia Akani.
Tnn., “Wana.”
Tnn., “Wana.”
Pia anaitwa Kalebu katika mstari wa 18, 19, na 42.
Pia anaitwa Kelubai katika mstari wa 9.
Tnn., “wana.”
Tnn., “wana.”
Tnn., “wana.”
Tnn., “Wana.”
Tnn., “wana.”
Pia anaitwa Kelubai katika mstari wa 9.