Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati 20:1-8

  • Jiji la Raba latekwa (1-3)

  • Majitu ya Wafilisti yauawa (4-8)

20  Mwanzoni mwa mwaka,* wakati ambapo wafalme huenda vitani, Yoabu+ aliwaongoza wanajeshi vitani, wakaiharibu nchi ya Waamoni; Yoabu akaenda na kuzingira Raba,+ lakini Daudi akabaki Yerusalemu.+ Yoabu alishambulia jiji la Raba na kulibomoa kabisa.+  Kisha Daudi akachukua taji lililokuwa kwenye kichwa cha Malkamu, akapata kwamba uzito wa taji hilo ulikuwa talanta moja* ya dhahabu, nalo lilikuwa na mawe yenye thamani; Daudi akavishwa taji hilo kichwani. Alichukua pia nyara nyingi sana kutoka katika jiji hilo.+  Akawatoa nje watu waliokuwa ndani yake, akawapa kazi+ ya kukata mawe kwa misumeno na kufanya kazi kwa vifaa vya chuma vyenye ncha kali na kwa mashoka. Hivyo ndivyo Daudi alivyofanya katika majiji yote ya Waamoni. Hatimaye Daudi na wanajeshi wote wakarudi Yerusalemu.  Baada ya hayo, wakapigana tena na Wafilisti kule Gezeri. Wakati huo Sibekai+ Mhusha alimuua Sipai, aliyekuwa mzao wa Warefaimu,+ nao wakatiishwa.  Wakapigana tena na Wafilisti, na Elhanani mwana wa Yairi akamuua Lahmi ndugu ya Goliathi+ Mgathi, aliyekuwa na mkuki wenye mpini kama mti wa wafumaji wa nguo.+  Vita vikatokea tena huko Gathi,+ ambako kulikuwa na mwanamume mkubwa isivyo kawaida,+ mwenye vidole 6 katika kila mkono na vidole 6 katika kila mguu, jumla ya vidole 24; naye pia alikuwa mzao wa Warefaimu.+  Aliendelea kuwadhihaki+ Waisraeli. Basi Yonathani mwana wa Shimea,+ ndugu ya Daudi, akamuua.  Watu hao walikuwa wazao wa Warefaimu+ huko Gathi,+ na Daudi na watumishi wake ndio waliowaua.

Maelezo ya Chini

Yaani, majira ya kuchipua.
Talanta moja ilikuwa na uzito wa kilogramu 34.2. Angalia Nyongeza B14.