Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati 21:1-30

  • Daudi awahesabu watu bila idhini (1-6)

  • Yehova awaadhibu (7-17)

  • Daudi ajenga madhabahu (18-30)

21  Kisha Shetani* akasimama dhidi ya Waisraeli na kumchochea Daudi awahesabu Waisraeli.+  Basi Daudi akamwambia Yoabu+ na wakuu wa watu: “Nendeni mkawahesabu Waisraeli kuanzia Beer-sheba mpaka Dani;+ kisha mniletee habari ili nijue idadi yao.”  Lakini Yoabu akasema: “Yehova na azidishe idadi ya watu wake mara 100! Bwana wangu mfalme, hao wote tayari ni watumishi wako bwana wangu, sivyo? Kwa nini bwana wangu unataka kufanya hivyo? Kwa nini uwafanye Waisraeli wawe na hatia?”  Lakini neno la mfalme likawa na nguvu kuliko neno la Yoabu. Basi Yoabu akaondoka na kusafiri kotekote Israeli, kisha akarudi Yerusalemu.+  Basi Yoabu akampa Daudi idadi ya watu walioandikishwa. Wanaume wote wa Israeli waliojihami kwa mapanga walikuwa 1,100,000, na wanaume wa Yuda waliojihami kwa mapanga walikuwa 470,000.+  Lakini hakuwaandikisha watu wa kabila la Lawi na Benjamini miongoni mwao,+ kwa sababu neno la mfalme lilimchukiza Yoabu.+  Basi jambo hilo halikumpendeza hata kidogo Mungu wa kweli, kwa hiyo akawaletea Waisraeli ugonjwa hatari.  Basi Daudi akamwambia Mungu wa kweli: “Nimetenda dhambi+ kubwa kwa kufanya jambo hili. Na sasa, tafadhali, nisamehe kosa langu mimi mtumishi wako,+ kwa maana nimetenda kwa upumbavu sana.”+  Kisha Yehova akamwambia hivi Gadi,+ mwonaji wa Daudi: 10  “Nenda ukamwambie Daudi, ‘Yehova anasema hivi: “Ninakupa mambo matatu ya kuchagua. Chagua jambo nitakalokutendea.”’” 11  Basi Gadi akaenda kwa Daudi na kumwambia, “Yehova anasema hivi: ‘Chagua 12  ikiwa unataka miaka mitatu ya njaa kali,+ au ikiwa unataka maadui wako wakufagilie mbali kwa miezi mitatu huku upanga wao ukikuandama,+ au siku tatu za upanga kutoka kwa Yehova—nchi ikumbwe na ugonjwa hatari+—huku malaika wa Yehova akileta maangamizi+ katika eneo lote la Israeli.’ Sasa fikiria jibu ninalopaswa kumpa Yule aliyenituma.” 13  Kwa hiyo Daudi akamwambia Gadi: “Jambo hilo linanihuzunisha sana. Tafadhali, acha nianguke mkononi mwa Yehova, kwa maana rehema zake ni nyingi sana;+ lakini usiniache nianguke mkononi mwa mwanadamu.”+ 14  Ndipo Yehova akaleta ugonjwa hatari+ Israeli hivi kwamba watu 70,000 miongoni mwa Waisraeli wakafa.+ 15  Zaidi ya hilo, Mungu wa kweli alimtuma malaika katika jiji la Yerusalemu ili kuliangamiza; lakini alipokuwa karibu kuliangamiza, Yehova akaona jambo hilo na kughairi* kwa sababu ya msiba huo,+ akamwambia malaika aliyekuwa akiwaangamiza watu: “Imetosha!+ Sasa shusha mkono wako.” Malaika wa Yehova alikuwa amesimama karibu na uwanja wa kupuria nafaka wa Ornani+ Myebusi.+ 16  Daudi alipoinua macho yake, alimwona malaika wa Yehova akiwa amesimama kati ya dunia na mbingu akiwa ameshika mkononi mwake upanga uliochomolewa+ na kuelekezwa Yerusalemu. Mara moja, Daudi na wazee, wakiwa wamevaa nguo za magunia,+ wakajiangusha chini kifudifudi.+ 17  Daudi akamwambia Mungu wa kweli: “Je, si mimi niliyesema watu wahesabiwe? Mimi ndiye niliyetenda dhambi, na mimi ndiye niliyekosea;+ lakini kondoo hawa—wamefanya nini? Ee Yehova Mungu wangu, tafadhali, acha mkono wako uniadhibu mimi na nyumba ya baba yangu; lakini usiwapige watu wako.”+ 18  Ndipo malaika wa Yehova akamwambia Gadi+ amwambie Daudi apande na kumjengea Yehova madhabahu kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Ornani Myebusi.+ 19  Basi Daudi akapanda kulingana na neno la Gadi, alilosema katika jina la Yehova. 20  Wakati huo, Ornani akageuka na kumwona huyo malaika, na wanawe wanne waliokuwa pamoja naye wakajificha. Wakati huo Ornani alikuwa akipura ngano. 21  Daudi alipopanda na kufika kwake, Ornani alitazama na kumwona Daudi, mara moja akatoka kwenye uwanja wa kupuria na kumwinamia Daudi kifudifudi. 22  Daudi akamwambia Ornani: “Niuzie* uwanja wa kupuria ili nimjengee Yehova madhabahu kwenye uwanja huo. Niuzie kwa bei kamili, ili ugonjwa hatari ambao umewakumba watu ukomeshwe.”+ 23  Lakini Ornani akamwambia Daudi: “Uchukue uwe wako, bwana wangu mfalme fanya lolote unaloona ni jema.* Tazama, ninatoa ng’ombe kwa ajili ya dhabihu za kuteketezwa na kifaa cha kupuria+ utakachotumia kama kuni na ngano ya toleo la nafaka. Ninatoa vitu hivi vyote.” 24  Hata hivyo, Mfalme Daudi akamwambia Ornani: “Hapana, ni lazima niununue kwa bei kamili, kwa sababu sitachukua kitu chako na kumpa Yehova au kutoa dhabihu za kuteketezwa ambazo hazinigharimu chochote.”+ 25  Basi Daudi akampimia Ornani shekeli 600 za dhahabu* kwa ajili ya uwanja huo. 26  Kisha Daudi akamjengea Yehova madhabahu+ mahali hapo na kutoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za ushirika, akasali kwa Yehova, ambaye sasa alimjibu kwa kushusha moto+ kutoka mbinguni kwenye madhabahu hiyo ya dhabihu za kuteketezwa. 27  Kisha Yehova akamwagiza yule malaika+ aurudishe upanga wake kwenye ala. 28  Wakati huo, Daudi alipoona kwamba Yehova amemjibu kwenye uwanja wa kupuria wa Ornani Myebusi, akaendelea kutoa dhabihu hapo. 29  Hata hivyo, lile hema la ibada la Yehova ambalo Musa alikuwa ametengeneza nyikani na ile madhabahu ya dhabihu za kuteketezwa vilikuwa mahali pa juu kule Gibeoni wakati huo.+ 30  Lakini Daudi hakuweza kwenda mbele yake ili kutafuta ushauri wa Mungu, kwa maana aliogopa upanga wa malaika wa Yehova.

Maelezo ya Chini

Au labda, “mpinzani.”
Au “kuhuzunika.”
Tnn., “Nipe.”
Tnn., “kilicho chema machoni pako.”
Shekeli moja ilikuwa na uzito wa gramu 11.4. Angalia Nyongeza B14.