Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati 25:1-31

  • Wanamuziki na waimbaji wa nyumba ya Mungu (1-31)

25  Isitoshe, Daudi na wakuu wa vikundi vya utumishi waliwatenga baadhi ya wana wa Asafu, Hemani, na Yeduthuni+ ili watoe unabii kwa kutumia vinubi, vinanda,+ na matoazi.+ Hii ndiyo orodha ya wanaume waliowekwa rasmi kwa ajili ya utumishi huo:  kutoka kwa wana wa Asafu: Zakuri, Yosefu, Nethania, na Asharela, wana wa Asafu waliokuwa chini ya usimamizi wa Asafu, aliyetoa unabii chini ya usimamizi wa mfalme.  Kutoka kwa Yeduthuni,+ wana wa Yeduthuni walikuwa: Gedalia, Zeri, Yeshaya, Shimei, Hashabia, na Matithia,+ wana sita, waliokuwa chini ya usimamizi wa Yeduthuni baba yao, aliyetoa unabii kwa kutumia kinubi, akimshukuru na kumsifu Yehova.+  Kutoka kwa Hemani,+ wana wa Hemani walikuwa: Bukia, Matania, Uzieli, Shebueli, Yerimothi, Hanania, Hanani, Eliatha, Gidalti, Romamti-ezeri, Yoshbekasha, Malothi, Hothiri, na Mahaziothi.  Hao wote walikuwa wana wa Hemani, mwonaji wa mfalme kuhusiana na mambo ya Mungu wa kweli ili kumtukuza;* basi Mungu wa kweli alimpa Hemani wana 14 na mabinti 3.  Hao wote walikuwa chini ya usimamizi wa baba yao wakiwa waimbaji katika nyumba ya Yehova, wakitumia matoazi, vinanda, na vinubi+ kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya Mungu wa kweli. Asafu, Yeduthuni, na Hemani walikuwa chini ya usimamizi wa mfalme.  Idadi yao pamoja na ndugu zao waliozoezwa kumwimbia Yehova, wote wakiwa stadi, ilikuwa 288.  Basi walipiga kura+ ili kupanga zamu zao, mdogo sawa na mkubwa, mwenye ustadi pamoja na mwanafunzi.  Kura ya kwanza ilimwangukia Asafu kwa ajili ya Yosefu,+ ya pili Gedalia+ (yeye na ndugu zake na wanawe walikuwa 12); 10  ya tatu Zakuri,+ wanawe na ndugu zake, 12; 11  ya nne Izri, wanawe na ndugu zake, 12; 12  ya tano Nethania,+ wanawe na ndugu zake, 12; 13  ya sita Bukia, wanawe na ndugu zake, 12; 14  ya saba Yesharela, wanawe na ndugu zake, 12; 15  ya nane Yeshaya, wanawe na ndugu zake, 12; 16  ya tisa Matania, wanawe na ndugu zake, 12; 17  ya kumi Shimei, wanawe na ndugu zake, 12; 18  ya 11 Azareli, wanawe na ndugu zake, 12; 19  ya 12 Hashabia, wanawe na ndugu zake, 12; 20  ya 13 Shubaeli,+ wanawe na ndugu zake, 12; 21  ya 14 Matithia, wanawe na ndugu zake, 12; 22  ya 15 Yeremothi, wanawe na ndugu zake, 12; 23  ya 16 Hanania, wanawe na ndugu zake, 12; 24  ya 17 Yoshbekasha, wanawe na ndugu zake, 12; 25  ya 18 Hanani, wanawe na ndugu zake, 12; 26  ya 19 Malothi, wanawe na ndugu zake, 12; 27  ya 20 Eliatha, wanawe na ndugu zake, 12; 28  ya 21 Hothiri, wanawe na ndugu zake, 12; 29  ya 22 Gidalti,+ wanawe na ndugu zake, 12; 30  ya 23 Mahaziothi,+ wanawe na ndugu zake, 12; 31  ya 24 Romamti-ezeri,+ wanawe na ndugu zake, 12.

Maelezo ya Chini

Tnn., “kuinua pembe yake.”