Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati 26:1-32

  • Vikundi vya walinzi wa malango (1-19)

  • Waweka hazina na maofisa wengine (20-32)

26  Hivi ndivyo vilivyokuwa vikundi vya walinzi:+ kutoka kwa Wakora, Meshelemia+ mwana wa Kore wa wana wa Asafu.  Na Meshelemia alikuwa na wana: Zekaria mzaliwa wa kwanza, wa pili Yediaeli, wa tatu Zebadia, wa nne Yathnieli,  wa tano Elamu, wa sita Yehohanani, wa saba Elieho-enai.  Na Obed-edomu alikuwa na wana: Shemaya mzaliwa wa kwanza, wa pili Yehozabadi, wa tatu Yoa, wa nne Sakari, wa tano Nethaneli,  wa sita Amieli, wa saba Isakari, na wa nane Peulethai; kwa maana Mungu alikuwa amembariki.  Na Shemaya mwana wake alizaa wana waliokuwa viongozi wa koo zao,* kwa maana walikuwa wanaume hodari wenye uwezo.  Wana wa Shemaya walikuwa: Othni, Refaeli, Obedi, na Elzabadi; na Elihu na Semakia ndugu zake, walikuwa wanaume wenye uwezo pia.  Hao wote walikuwa wazao wa wana wa Obed-edomu; wao pamoja na wana wao na ndugu zao walikuwa wanaume wenye uwezo waliostahili kwa ajili ya utumishi huo, watu 62 wa Obed-edomu.  Na Meshelemia+ alikuwa na wana na ndugu, wanaume 18 wenye uwezo. 10  Na Hosa wa wana wa Merari alikuwa na wana. Shimri ndiye aliyekuwa kiongozi, kwa maana ingawa hakuwa mzaliwa wa kwanza, baba yake alimweka kuwa kiongozi, 11  wa pili Hilkia, wa tatu Tebalia, wa nne Zekaria. Wana wote wa Hosa na ndugu zake walikuwa 13. 12  Katika vikundi hivyo vya walinzi wa malango, viongozi walikuwa na kazi kama za ndugu zao, kuhudumu katika nyumba ya Yehova. 13  Kwa hiyo walipiga kura,+ mdogo sawa na mkubwa kulingana na koo zao,* kwa ajili ya malango mbalimbali. 14  Kura ya upande wa mashariki ilimwangukia Shelemia. Wakapiga kura kwa ajili ya Zekaria mwanawe, mshauri mwenye busara, aliangukiwa na kura ya upande wa kaskazini. 15  Obed-edomu alipata kura ya upande wa kusini, na wanawe+ walipewa kazi ya maghala. 16  Shupimu na Hosa+ walipata kura ya upande wa magharibi, karibu na Lango la Shalekethi kando ya barabara kuu inayoelekea juu, kikundi cha ulinzi karibu na kikundi kingine cha ulinzi; 17  kulikuwa na Walawi sita upande wa mashariki; wanne kila siku upande wa kaskazini, na wanne kila siku upande wa kusini; na kwenye maghala,+ wawili wawili; 18  kwa ajili ya baraza upande wa magharibi, kulikuwa na wanne kwenye barabara kuu+ na wawili barazani. 19  Hivyo ndivyo vilivyokuwa vikundi vya walinzi wa malango vya wana wa Wakora na wa Wamerari. 20  Kuhusu Walawi, Ahiya alisimamia hazina za nyumba ya Mungu wa kweli na hazina za vitu vilivyofanywa kuwa vitakatifu.*+ 21  Wana wa Ladani: wana wa Mgershoni mwana wa Ladani, viongozi wa koo* za Ladani Mgershoni, kulikuwa na Yehieli+ 22  na wana wa Yehieli, Zethamu na Yoeli ndugu yake. Walisimamia hazina za nyumba ya Yehova.+ 23  Kutoka kwa Waamramu, Waishari, Wahebroni, na Wauzieli,+ 24  Shebueli mwana wa Gershomu mwana wa Musa alikuwa kiongozi aliyesimamia maghala. 25  Na kuhusu ndugu zake, kutoka kwa Eliezeri+ kulikuwa na Rehabia+ mwana wa Eliezeri, Yeshaya mwana wa Rehabia, Yoramu mwana wa Yeshaya, Zikri mwana wa Yoramu, na Shelomothi mwana wa Zikri. 26  Huyu Shelomothi na ndugu zake walisimamia hazina zote za vitu vilivyofanywa kuwa vitakatifu,+ ambavyo Mfalme Daudi,+ viongozi wa koo,*+ wakuu wa maelfu na wa mamia, na wakuu wa jeshi walikuwa wamevifanya kuwa vitakatifu. 27  Baadhi ya vitu walivyopata vitani+ na baadhi ya nyara+ walizifanya kuwa takatifu ili kuidumisha nyumba ya Yehova; 28  pia, vitu vyote ambavyo Samweli mwonaji,+ Sauli mwana wa Kishi, Abneri+ mwana wa Neri, na Yoabu+ mwana wa Seruya+ walikuwa wamevifanya kuwa vitakatifu. Kitu chochote ambacho mtu yeyote alikifanya kuwa kitakatifu kiliwekwa chini ya usimamizi wa Shelomithi na ndugu zake. 29  Kutoka kwa Waishari,+ Kenania na wanawe walipewa kazi za nje za usimamizi wakiwa maofisa na waamuzi+ wa Israeli. 30  Kutoka kwa Wahebroni,+ Hashabia na ndugu zake, wanaume 1,700 wenye uwezo, waliwasimamia wakuu wa Israeli katika eneo lililokuwa upande wa magharibi wa Yordani kuhusiana na kazi zote za Yehova na utumishi wa mfalme. 31  Kutoka kwa Wahebroni, Yeriya+ alikuwa kiongozi wa Wahebroni kulingana na nasaba ya ukoo wao.* Katika mwaka wa 40 wa utawala wa Daudi,+ walitafutwa, na wanaume hodari wenye uwezo wakapatikana miongoni mwao kule Yazeri,+ Gileadi. 32  Na ndugu zake walikuwa 2,700, wanaume wenye uwezo, viongozi wa koo.* Basi Mfalme Daudi akawaweka wawasimamie watu wa kabila la Rubeni, Gadi, na nusu ya kabila la Manase, katika kila jambo la Mungu wa kweli na la mfalme.

Maelezo ya Chini

Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Au “vitu vilivyowekwa wakfu.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.