Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati 3:1-24

  • Wazao wa Daudi (1-9)

  • Uzao wa kifalme wa Daudi (10-24)

3  Hawa ndio wana wa Daudi waliozaliwa Hebroni:+ mzaliwa wa kwanza aliitwa Amnoni,+ mama yake aliitwa Ahinoamu+ kutoka Yezreeli; wa pili, Danieli, mama yake aliitwa Abigaili+ Mkarmeli;  wa tatu, Absalomu,+ mwana wa Maaka binti ya Talmai mfalme wa Geshuri; wa nne, Adoniya+ mwana wa Hagithi;  wa tano, Shefatia, ambaye mama yake aliitwa Abitali; na wa sita, Ithreamu, ambaye mama yake aliitwa Egla, mke wa Daudi.  Aliwazaa wana hao sita kule Hebroni; alitawala huko kwa miaka 7 na miezi 6, naye alitawala kule Yerusalemu kwa miaka 33.+  Aliwazaa wana wafuatao huko Yerusalemu:+ Shimea, Shobabu, Nathani,+ na Sulemani;+ mama ya wana hao wanne alikuwa Bath-sheba+ binti ya Amieli.  Alikuwa na wana wengine tisa ambao ni Ibhari, Elishama, Elifeleti,  Noga, Nefegi, Yafia,  Elishama, Eliada, na Elifeleti.  Hao wote walikuwa wana wa Daudi, bila kuhesabu wana wa masuria, na dada yao alikuwa Tamari.+ 10  Mwana wa Sulemani alikuwa Rehoboamu;+ mwana wa Rehoboamu alikuwa Abiya,+ mwana wa Abiya alikuwa Asa,+ mwana wa Asa alikuwa Yehoshafati,+ 11  mwana wa Yehoshafati alikuwa Yehoramu,+ mwana wa Yehoramu alikuwa Ahazia,+ mwana wa Ahazia alikuwa Yehoashi,+ 12  mwana wa Yehoashi alikuwa Amazia,+ mwana wa Amazia alikuwa Azaria,+ mwana wa Azaria alikuwa Yothamu,+ 13  mwana wa Yothamu alikuwa Ahazi,+ mwana wa Ahazi alikuwa Hezekia,+ mwana wa Hezekia alikuwa Manase,+ 14  mwana wa Manase alikuwa Amoni,+ mwana wa Amoni alikuwa Yosia.+ 15  Wana wa Yosia walikuwa Yohanani mzaliwa wa kwanza, wa pili, Yehoyakimu,+ wa tatu, Sedekia,+ wa nne, Shalumu. 16  Wana wa Yehoyakimu walikuwa Yekonia+ mwanawe na Sedekia mwana wa Yekonia. 17  Wana wa Yekonia aliyekuwa mfungwa walikuwa Shealtieli, 18  Malkiramu, Pedaya, Shenazari, Yekamia, Hoshama, na Nedabia. 19  Wana wa Pedaya walikuwa Zerubabeli+ na Shimei; na wana wa Zerubabeli walikuwa Meshulamu na Hanania (na dada yao alikuwa Shelomithi); 20  naye alikuwa na wana wengine watano ambao ni Hashuba, Oheli, Berekia, Hasadia, na Yushab-hesedi. 21  Wana wa Hanania walikuwa Pelatia na Yeshaya; mwana* wa Yeshaya alikuwa Refaya; mwana* wa Refaya alikuwa Arnani; mwana* wa Arnani alikuwa Obadia; mwana* wa Obadia alikuwa Shekania; 22  na wana wa Shekania walikuwa Shemaya na wana wa Shemaya walikuwa Hatushi, Igali, Baria, Nearia, na Shafati—jumla ya wana sita. 23  Na wana wa Nearia walikuwa Elioenai, Hizkia, na Azrikamu, wana watatu. 24  Na wana wa Elioenai walikuwa Hodavia, Eliashibu, Pelaya, Akubu, Yohanani, Delaya, na Anani, wana saba.

Maelezo ya Chini

Tnn., “wana.”
Tnn., “wana.”
Tnn., “wana.”
Tnn., “wana.”