Kitabu cha Kwanza cha Samweli 4:1-22

  • Wafilisti wateka sanduku la agano (1-11)

  • Eli na wanawe wafa (12-22)

4  Na neno la Samweli likawafikia Waisraeli wote. Kisha Waisraeli wakaenda kupigana na Wafilisti; wakapiga kambi kando ya Ebenezeri, na Wafilisti walikuwa wamepiga kambi Afeki.  Wafilisti wakajipanga kivita ili kupigana na Waisraeli, lakini mambo yakawaendea vibaya Waisraeli vitani, nao wakashindwa na Wafilisti, ambao waliwaua wanaume wapatao 4,000 kwenye uwanja wa vita.  Watu waliporudi kambini, wazee wa Israeli wakasema hivi: “Kwa nini Yehova ameruhusu tushindwe leo na Wafilisti?*+ Na tujichukulie sanduku la agano la Yehova kutoka Shilo,+ twende nalo ili lituokoe kutoka mikononi mwa maadui wetu.”  Basi watu wakawatuma wanaume kwenda Shilo, nao wakachukua kutoka huko sanduku la agano la Yehova wa majeshi, anayeketi akiwa mfalme juu ya* makerubi.+ Na wana wawili wa Eli, yaani, Hofni na Finehasi,+ walikuwa huko pia pamoja na sanduku la agano la Mungu wa kweli.  Mara tu sanduku la agano la Yehova lilipofika kambini, Waisraeli wote wakaanza kupiga kelele kwa sauti kubwa, hivi kwamba dunia ikatikisika.  Wafilisti waliposikia kelele hizo, wakasema: “Kwa nini kuna kelele nyingi sana katika kambi ya Waebrania?” Hatimaye wakapata habari kwamba Sanduku la Yehova lilikuwa limeletwa kambini.  Wafilisti wakaogopa, kwa sababu walisema: “Mungu amekuja kambini!”+ Basi wakasema: “Ole wetu, kwa maana jambo kama hili halijawahi kamwe kutokea!  Ole wetu! Ni nani atakayetuokoa kutoka katika mkono wa Mungu huyu mkuu? Huyu ndiye Mungu aliyewachinja Wamisri kwa kila aina ya mapigo nyikani.+  Iweni jasiri na kutenda kama wanaume, enyi Wafilisti, ili msiwatumikie Waebrania kama walivyowatumikia ninyi.+ Tendeni kama wanaume, mkapigane!” 10  Basi Wafilisti wakapigana nao, na Waisraeli wakashindwa,+ na kila mmoja wao akakimbilia katika hema lake. Yalikuwa mauaji makubwa sana; wanajeshi 30,000 wa Israeli wanaotembea kwa miguu waliuawa. 11  Isitoshe, Sanduku la Mungu lilitekwa, na wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi, wakafa.+ 12  Mtu fulani Mbenjamini akakimbia kutoka katika uwanja wa vita, akafika Shilo siku hiyo akiwa amevaa nguo zilizoraruka na akiwa na mavumbi kichwani.+ 13  Mtu huyo alipofika, Eli alikuwa ameketi kwenye kiti kando ya barabara akitazama barabarani, kwa kuwa moyo wake ulikuwa ukitetemeka kwa sababu ya Sanduku la Mungu wa kweli.+ Mtu huyo akaingia jijini kutangaza habari hizo, na jiji lote likaanza kulia kwa sauti kubwa. 14  Eli aliposikia vilio hivyo, akauliza: “Kelele hizo za machafuko ni za nini?” Mtu huyohuyo akafika haraka na kumwambia Eli habari hizo. 15  (Wakati huo Eli alikuwa na umri wa miaka 98, naye alikodoa macho yake mbele, lakini hakuweza kuona.)+ 16  Kisha mtu huyo akamwambia Eli: “Ni mimi niliyetoka katika uwanja wa vita! Nimekimbia kutoka katika uwanja wa vita leo hii.” Basi akamuuliza: “Mwanangu, ilikuwaje?” 17  Basi mtu huyo aliyeleta habari akasimulia hivi: “Waisraeli wamewakimbia Wafilisti, na watu wameshindwa vibaya sana;+ pia, wana wako wawili, Hofni na Finehasi, wamekufa,+ na Sanduku la Mungu wa kweli limetekwa.”+ 18  Mara tu alipotaja Sanduku la Mungu wa kweli, Eli akaanguka nyuma kutoka kwenye kiti chake kando ya lango, na shingo yake ikavunjika naye akafa, kwa sababu alikuwa amezeeka na alikuwa mzito. Alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka 40. 19  Binti mkwe wake, yaani, mke wa Finehasi, alikuwa mjamzito naye alikuwa karibu kuzaa. Aliposikia kwamba Sanduku la Mungu wa kweli limetekwa na kwamba baba mkwe wake na mume wake wamekufa, akainama na kwa ghafla akapata uchungu wa kuzaa, kisha akazaa. 20  Alipokuwa akifa, wanawake waliokuwa wamesimama kando yake wakasema: “Usiogope, kwa maana umezaa mwana.” Hakujibu wala kukazia fikira jambo hilo.* 21  Lakini alimwita mvulana huyo Ikabodi,*+ akisema: “Utukufu umeondoka Israeli na kwenda uhamishoni,”+ alisema hivyo kwa sababu Sanduku la Mungu wa kweli lilitekwa na kwa sababu ya mambo yaliyompata baba mkwe wake na mume wake.+ 22  Basi akasema: “Utukufu umeondoka Israeli na kwenda uhamishoni, kwa sababu Sanduku la Mungu wa kweli limetekwa.”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “Kwa nini Yehova ametushinda leo kwa kuwatumia Wafilisti?”
Au labda, “katikati ya.”
Au “wala kutia moyoni jambo hilo.”
Maana yake “Utukufu uko Wapi?”