Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati 10:1-19

  • Waisraeli wamwasi Rehoboamu (1-19)

10  Rehoboamu alienda Shekemu,+ kwa maana Waisraeli wote walikuwa wamekuja Shekemu kumfanya kuwa mfalme.+  Mara tu Yeroboamu+ mwana wa Nebati aliposikia habari hizo (bado alikuwa akiishi Misri kwa sababu alikuwa amemkimbia Mfalme Sulemani),+ akarudi kutoka Misri.  Ndipo wakawatuma watu waende kumwita, kisha Yeroboamu na Waisraeli wote wakaja kwa Rehoboamu na kumwambia hivi:  “Baba yako aliifanya nira yetu kuwa nzito.+ Lakini ukiufanya utumishi mzito wa baba yako kuwa mwepesi zaidi na kupunguza nira nzito* aliyotutwika, tutakutumikia.”  Ndipo akawaambia: “Rudini kwangu baada ya siku tatu.” Basi watu wakaenda zao.+  Kisha Mfalme Rehoboamu akashauriana na wanaume wazee waliomtumikia Sulemani baba yake alipokuwa hai, akawauliza: “Mnanishauri niwape jibu gani watu hawa?”  Wakamjibu: “Ukiwa mwema kwa watu hawa na kuwafurahisha na kuwapa jibu linalofaa, watakuwa watumishi wako sikuzote.”  Hata hivyo, alikataa ushauri aliopewa na wanaume wazee, akashauriana na vijana wa rika lake na ambao sasa walikuwa watumishi wake.+  Aliwauliza: “Mnashauri tuwape jibu gani watu hawa ambao wameniambia, ‘Ifanye nira ambayo baba yako alitutwika iwe nyepesi zaidi’?” 10  Vijana hao wa rika lake wakamwambia: “Hivi ndivyo unavyopaswa kuwaambia watu waliokwambia, ‘Baba yako aliifanya nira yetu kuwa nzito, lakini wewe unapaswa kuifanya kuwa nyepesi zaidi kwa ajili yetu’; hivi ndivyo unavyopaswa kuwaambia, ‘Kidole changu kidogo kitakuwa kinene kuliko kiuno cha baba yangu. 11  Baba yangu aliwatwika nira nzito, lakini mimi nitazidisha uzito wa nira yenu. Baba yangu aliwaadhibu kwa mijeledi, lakini mimi nitawaadhibu kwa mijeledi yenye miiba.’” 12  Yeroboamu na watu wote wakaja kwa Rehoboamu siku ya tatu, kama mfalme alivyokuwa amesema: “Rudini kwangu siku ya tatu.”+ 13  Lakini mfalme akawajibu kwa ukali. Kwa hiyo Mfalme Rehoboamu akakataa ushauri wa wanaume wazee. 14  Akawajibu kama alivyoshauriwa na vijana wa rika lake, na kusema: “Nitafanya nira yenu iwe nzito zaidi, nami nitazidisha uzito wake. Baba yangu aliwaadhibu kwa mijeledi, lakini mimi nitawaadhibu kwa mijeledi yenye miiba.” 15  Basi mfalme hakuwasikiliza watu, kwa sababu Mungu wa kweli ndiye aliyesababisha badiliko hilo la mambo,+ ili atimize neno ambalo Yehova alimwambia Yeroboamu mwana wa Nebati kupitia Ahiya Mshilo.+ 16  Waisraeli wote walipoona kwamba mfalme amekataa kuwasikiliza, wakamwambia hivi mfalme: “Tuna ushirika gani na Daudi? Hatuna urithi wowote katika mwana wa Yese. Kila mtu aende kwa miungu yake, enyi Waisraeli! Sasa itunze nyumba yako mwenyewe, Ee Daudi.”+ Ndipo Waisraeli wote wakarudi katika nyumba zao.*+ 17  Lakini Rehoboamu akaendelea kuwatawala Waisraeli walioishi katika majiji ya Yuda.+ 18  Kisha Mfalme Rehoboamu akamtuma Hadoramu,+ aliyekuwa msimamizi wa watu waliofanya kazi ya kulazimishwa, lakini Waisraeli wote wakamuua kwa kumpiga mawe. Mfalme Rehoboamu akafaulu kupanda gari lake na kukimbilia Yerusalemu.+ 19  Na tangu siku hiyo Waisraeli wamekuwa wakiiasi nyumba ya Daudi.

Maelezo ya Chini

Au “inayokandamiza.”
Tnn., “mahema yao.”