Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati 11:1-23

  • Utawala wa Rehoboamu (1-12)

  • Walawi washikamanifu wahamia Yuda (13-17)

  • Familia ya Rehoboamu (18-23)

11  Rehoboamu alipofika Yerusalemu, mara moja aliikusanya nyumba ya Yuda na kabila la Benjamini,+ mashujaa 180,000 waliozoezwa,* ili wapigane na Waisraeli na kuurudisha ufalme kwa Rehoboamu.+  Kisha neno hili la Yehova likamjia Shemaya+ mtu wa Mungu wa kweli:  “Mwambie Rehoboamu mwana wa Sulemani mfalme wa Yuda na Waisraeli wote walio Yuda na Benjamini,⁠  ‘Hivi ndivyo Yehova anavyosema: “Msipande kwenda kupigana na ndugu zenu. Kila mmoja wenu arudi nyumbani kwake, kwa maana nimesababisha mambo haya yatukie.”’”+ Basi wakalitii neno la Yehova na kurudi, nao hawakwenda kupigana na Yeroboamu.  Rehoboamu aliishi Yerusalemu na kujenga majiji yenye ngome huko Yuda.⁠  Basi akajenga* Bethlehemu,+ Etamu, Tekoa,+  Beth-suri, Soko,+ Adulamu,+  Gathi,+ Maresha, Zifu,+  Adoraimu, Lakishi,+ Azeka,+ 10  Sora, Aiyaloni,+ na Hebroni,+ majiji yenye ngome yaliyokuwa Yuda na Benjamini. 11  Pia, aliimarisha maeneo yenye ngome, akawaweka makamanda humo na kuwapa chakula na mafuta na divai, 12  naye akapeleka ngao kubwa na mikuki katika majiji yote mbalimbali; akayaimarisha kwa kiwango kikubwa sana. Na majiji ya Yuda na Benjamini yakaendelea kuwa yake. 13  Na makuhani na Walawi waliokuwa katika nchi yote ya Israeli wakamuunga mkono, wakaja kutoka katika maeneo yao yote. 14  Walawi waliacha malisho yao na miliki yao+ wakaja Yuda na Yerusalemu, kwa sababu Yeroboamu na wanawe walikuwa wamewaondoa ili wasiwe makuhani wa Yehova.+ 15  Kisha Yeroboamu akawaweka makuhani wake mwenyewe ili wahudumu mahali pa juu+ na kuwatumikia roho waovu wenye umbo la mbuzi*+ na ndama aliokuwa ametengeneza.+ 16  Na watu kutoka katika makabila yote ya Israeli waliokuwa wameazimia moyoni mwao kumtafuta Yehova Mungu wa Israeli wakawafuata mpaka Yerusalemu ili kumtolea dhabihu Yehova Mungu wa mababu zao.+ 17  Kwa miaka mitatu waliuimarisha ufalme wa Yuda na kumuunga mkono Rehoboamu mwana wa Sulemani, kwa maana walitembea katika njia ya Daudi na Sulemani kwa miaka mitatu. 18  Kisha Rehoboamu akamwoa Mahalathi binti ya Yerimothi mwana wa Daudi na wa Abihaili binti ya Eliabu+ mwana wa Yese. 19  Baada ya muda akamzalia wana hawa: Yeushi, Shemaria, na Zahamu. 20  Kisha akamwoa Maaka mjukuu wa Absalomu.+ Baada ya muda akamzalia Abiya,+ Atai, Ziza, na Shelomithi. 21  Rehoboamu alimpenda zaidi Maaka mjukuu wa Absalomu kuliko wake zake wengine wote na masuria+ wake, kwa maana alikuwa na wake 18 na masuria 60, naye akawazaa wana 28 na mabinti 60. 22  Kwa hiyo Rehoboamu akamweka Abiya mwana wa Maaka kuwa mkuu na kiongozi miongoni mwa ndugu zake, kwa maana alikusudia kumweka kuwa mfalme. 23  Hata hivyo, alitenda kwa busara* na kuwatuma* baadhi ya wanawe kwenye maeneo yote ya Yuda na Benjamini, kwenye majiji yote yenye ngome,+ akawapa chakula kingi na kuwatafutia wake wengi.

Maelezo ya Chini

Tnn., “waliochaguliwa.”
Au “akaimarisha.”
Tnn., “mbuzi.”
Tnn., “uelewaji.”
Au “kuwasambaza.”