Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati 14:1-15

  • Kifo cha Abiya (1)

  • Asa, mfalme wa Yuda (2-8)

  • Asa awashinda Waethiopia 1,000,000 (9-15)

14  Kisha Abiya akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake katika Jiji la Daudi;+ na Asa mwanawe akawa mfalme baada yake. Katika siku zake nchi ilikuwa na amani* kwa miaka kumi.  Asa alitenda yaliyokuwa mema na sawa machoni pa Yehova Mungu wake.  Aliondoa madhabahu za kigeni+ na mahali pa juu, akazivunjavunja nguzo takatifu,+ na kuikata miti mitakatifu.*+  Zaidi ya hayo, aliwaambia watu wa Yuda wamtafute Yehova Mungu wa mababu zao na kushika Sheria na amri.  Kwa hiyo aliondoa mahali pa juu na vinara vya uvumba+ katika majiji yote ya Yuda, na chini ya utawala wake ufalme uliendelea kuwa bila usumbufu.  Alijenga majiji yenye ngome huko Yuda,+ kwa kuwa nchi haikuwa na usumbufu na hakuna yeyote aliyepigana vita naye katika miaka hiyo, kwa maana Yehova alimpumzisha.+  Aliwaambia hivi watu wa Yuda: “Na tujenge majiji haya na kuyazingira kwa kuta na minara,+ malango* na makomeo. Kwa maana nchi bado imo mikononi mwetu kwa sababu tumemtafuta Yehova Mungu wetu. Tumemtafuta, naye ametupumzisha pande zote.” Kwa hiyo kazi yao ya ujenzi ilifanikiwa.+  Asa alikuwa na jeshi la wanaume 300,000 waliokuwa na ngao kubwa na mikuki. Na kutoka Benjamini kulikuwa na mashujaa hodari 280,000 waliobeba ngao ndogo* na kujihami kwa pinde.*+  Baadaye Zera Mwethiopia akaja kupigana nao akiwa na jeshi la wanaume 1,000,000 na magari 300 ya vita.+ Alipofika Maresha,+ 10  Asa akaenda kupigana naye, na Asa na jeshi lake wakajipanga kivita katika Bonde la Sefatha huko Maresha. 11  Kisha Asa akamlilia Yehova Mungu wake+ akisema: “Ee Yehova, haijalishi kwako ikiwa wale unaowasaidia ni wengi au hawana nguvu.+ Tusaidie, Ee Yehova Mungu wetu, kwa maana tunakutegemea* wewe,+ na katika jina lako tumekuja kupigana na umati huu.+ Ee Yehova, wewe ni Mungu wetu. Usiache mwanadamu anayeweza kufa akushinde.”+ 12  Kwa hiyo Yehova akawashinda Waethiopia mbele ya Asa na mbele ya watu wa Yuda, na Waethiopia wakakimbia.+ 13  Asa na watu waliokuwa pamoja naye wakawafuatia mpaka Gerari,+ nao wakaendelea kuwaua Waethiopia hivi kwamba hakuna hata mmoja wao aliyebaki hai, kwa maana walipondwapondwa na Yehova na jeshi lake. Kisha wakachukua nyara nyingi sana. 14  Zaidi ya hayo, waliyashambulia majiji yote yaliyozunguka Gerari, kwa maana hofu ya Yehova ilikuwa imewashika wakaaji wa majiji hayo; nao wakapora majiji yote, kwa kuwa kulikuwa na vitu vingi vya kuporwa katika majiji hayo. 15  Walishambulia pia mahema ya wale waliokuwa na mifugo, wakateka idadi kubwa ya kondoo na ngamia, kisha wakarudi Yerusalemu.

Maelezo ya Chini

Tnn., “ilipumzika.”
Angalia Kamusi.
Tnn., “milango miwili-miwili.”
Tnn., “kukanyaga upinde.”
Kwa kawaida ilibebwa na wapiga mishale.
Tnn., “tunakuegemea.”