Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati 2:1-18

  • Matayarisho ya kujenga hekalu (1-18)

2  Basi Sulemani akaagiza nyumba ijengwe kwa ajili ya jina la Yehova+ na nyumba* kwa ajili ya ufalme wake.+  Sulemani akawaandikisha wanaume 70,000 kuwa vibarua,* wanaume 80,000 kuwa wakataji wa mawe milimani,+ na wanaume 3,600 kuwa waangalizi wao.+  Pia, Sulemani akamtumia Hiramu+ mfalme wa Tiro ujumbe huu: “Nifanyie kama ulivyomfanyia Daudi baba yangu ulipomletea mbao za mierezi ili ajenge nyumba ya* kuishi.+  Sasa ninajenga nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wangu, ili niitakase kwake, nifukize uvumba wenye manukato+ mbele zake, na pia kwa ajili ya mikate ya tabaka* inayotolewa daima+ na pia dhabihu za kuteketezwa, asubuhi na jioni,+ nyakati za Sabato,+ miezi mipya,+ na kwenye majira ya sherehe+ za Yehova Mungu wetu. Huu ni wajibu wa kudumu kwa Waisraeli.  Nyumba nitakayojenga itakuwa kuu, kwa maana Mungu wetu ni mkuu kuliko miungu mingine yote.  Na ni nani anayeweza kumjengea nyumba? Kwa maana mbingu na mbingu za mbingu haziwezi kumtosha,+ basi mimi ni nani hivi kwamba nimjengee nyumba isipokuwa iwe mahali pa kufukizia moshi wa dhabihu mbele zake?  Sasa niletee fundi aliye na ustadi wa kutengeneza vitu kwa kutumia dhahabu, fedha, shaba,+ chuma, sufu ya zambarau, nyuzi nyekundu, na nyuzi za bluu, na ambaye anajua kuchonga. Atafanya kazi Yuda na Yerusalemu pamoja na mafundi wangu stadi, ambao Daudi baba yangu aliwachagua.+  Nawe uniletee mbao za mierezi, miberoshi,+ na misandali+ kutoka Lebanoni, kwa maana najua vizuri kwamba watumishi wako wana uzoefu wa kukata miti ya Lebanoni.+ Watumishi wangu watafanya kazi pamoja na watumishi wako+  ili wanitayarishie mbao nyingi sana, kwa maana nyumba nitakayojenga itakuwa na ukuu usio wa kawaida. 10  Sasa tazama! Nitawaletea chakula watumishi wako,+ yaani, wapasua mbao wanaokata miti: nitawaletea kori 20,000 za ngano, kori 20,000* za shayiri, bathi 20,000 za divai, na bathi 20,000* za mafuta.” 11  Ndipo Hiramu mfalme wa Tiro akatuma barua hii kwa Sulemani: “Kwa sababu Yehova anawapenda watu wake, amekuweka kuwa mfalme wao.” 12  Kisha Hiramu akasema: “Na asifiwe Yehova Mungu wa Israeli, aliyeziumba mbingu na dunia, kwa sababu amempa Mfalme Daudi mwana mwenye hekima,+ aliyebarikiwa kuwa na busara na uelewaji,+ atakayejenga nyumba kwa ajili ya Yehova na nyumba kwa ajili ya ufalme wake. 13  Sasa namtuma fundi stadi, aliyebarikiwa kuwa na uelewaji, Hiram-abi,+ 14  mwana wa mwanamke wa kabila la Dani, lakini baba yake alikuwa Mtiro; ana uzoefu wa kutengeneza vitu kwa kutumia dhahabu, fedha, shaba, chuma, mawe, mbao, sufu ya zambarau, nyuzi za bluu, kitambaa bora, na nyuzi nyekundu.+ Anaweza kuchonga michongo ya kila aina na kubuni na kutengeneza kitu chochote anachoambiwa.+ Atafanya kazi pamoja na mafundi wako stadi na mafundi stadi wa bwana wangu Daudi baba yako. 15  Sasa bwana wangu tutumie ngano, shayiri, mafuta, na divai uliyotuahidi sisi watumishi wako.+ 16  Nasi tutakata miti kutoka Lebanoni,+ idadi yoyote unayohitaji, nasi tutakuletea magogo hayo yakiwa mafungu-mafungu ili yaelee baharini mpaka Yopa;+ nawe utayapeleka Yerusalemu.”+ 17  Kisha Sulemani akawahesabu wanaume wote waliokuwa wakaaji wageni katika nchi ya Israeli,+ baada ya ile hesabu ya watu ambayo Daudi baba yake alikuwa amechukua,+ wakapatikana wanaume 153,600. 18  Kwa hiyo akawaweka watu 70,000 kati yao kuwa vibarua,* 80,000 kuwa wakataji wa mawe+ milimani, na 3,600 kuwa waangalizi wa kuhakikisha kwamba watu wanafanya kazi.+

Maelezo ya Chini

Au “jumba la mfalme.”
Au “wabeba mizigo.”
Au “jumba la mfalme la.”
Yaani, mikate ya wonyesho.
Kori moja ilikuwa sawa na lita 220 (kilogramu 170 hivi). Angalia Nyongeza B14.
Bathi ilikuwa sawa na lita 22. Angalia Nyongeza B14.
Au “wabeba mizigo.”