Kitabu cha Pili cha Samweli 8:1-18

  • Ushindi mbalimbali wa Daudi (1-14)

  • Wakuu katika utawala wa Daudi (15-18)

8  Baadaye, Daudi aliwashinda Wafilisti+ na kuwatiisha,+ akachukua jiji la Metheg-ama kutoka mikononi mwa Wafilisti.  Akawashinda Wamoabu+ na kuwaamuru walale chini ardhini, naye akawapima kwa kamba. Alipima safu mbili za watu ambao wangeuawa, na safu moja nzima ya watu ambao hawangeuawa.+ Wamoabu wakawa watumishi wa Daudi na kumletea ushuru.+  Daudi alimshinda Hadadezeri mwana wa Rehobu mfalme wa Soba+ mfalme huyo alipokuwa akienda kurudisha mamlaka yake katika eneo la Mto Efrati.+  Daudi akawateka wapanda farasi 1,700 na wanajeshi wake 20,000 wanaotembea kwa miguu. Kisha Daudi akawakata farasi wote mishipa ya miguu isipokuwa farasi 100 waliokokota magari.+  Wasiria wa Damasko+ walipokuja kumsaidia Mfalme Hadadezeri wa Soba, Daudi aliwaua Wasiria 22,000.+  Halafu Daudi akaweka kambi za kijeshi kule Siria ya Damasko, na Wasiria wakawa watumishi wa Daudi na kumletea ushuru. Yehova alimpa Daudi ushindi* popote alipoenda.+  Isitoshe, Daudi alichukua ngao za mviringo za dhahabu kutoka kwa watumishi wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu.+  Mfalme Daudi alichukua shaba nyingi sana kutoka Beta na Berothai, majiji ya Hadadezeri.  Basi Mfalme Toi wa Hamathi+ akasikia kwamba Daudi alikuwa amelishinda jeshi lote la Hadadezeri.+ 10  Kwa hiyo Toi akamtuma Yoramu mwana wake kwa Mfalme Daudi ili amjulie hali na kumpongeza kwa sababu alikuwa amepigana na Hadadezeri na kumshinda (kwa maana mara nyingi Hadadezeri alimshambulia Toi); na Yoramu alimletea Daudi vitu vya fedha, dhahabu, na shaba. 11  Mfalme Daudi akavitakasa vitu hivyo ili viwe vya Yehova, pamoja na fedha na dhahabu aliyotakasa kutoka kwa mataifa yote aliyokuwa ameyashinda:+ 12  kutoka Siria na kutoka Moabu,+ kutoka kwa Waamoni, Wafilisti,+ Waamaleki,+ na kutoka katika nyara za Hadadezeri+ mwana wa Rehobu mfalme wa Soba. 13  Pia Daudi alijijengea jina aliporudi baada ya kuwaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.+ 14  Aliweka kambi za kijeshi huko Edomu. Aliweka kambi za kijeshi katika nchi yote ya Edomu, na Waedomu wote wakawa watumishi wa Daudi.+ Yehova alimpa Daudi ushindi* popote alipoenda.+ 15  Daudi akaendelea kutawala Israeli yote,+ naye aliwatawala watu wake wote+ kwa haki na uadilifu.+ 16  Yoabu+ mwana wa Seruya alikuwa mkuu wa jeshi, na Yehoshafati+ mwana wa Ahiludi alifanya kazi ya kuweka kumbukumbu. 17  Sadoki+ mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani, na Seraya alikuwa mwandishi. 18  Benaya+ mwana wa Yehoyada aliwasimamia Wakerethi na Wapelethi.+ Na wana wa Daudi walikuwa wahudumu wakuu.*

Maelezo ya Chini

Au “wokovu.”
Au “wokovu.”
Tnn., “walikuwa makuhani.”