Kitabu cha Pili cha Wafalme 11:1-21

  • Athalia aunyakua ufalme (1-3)

  • Yehoashi awekwa kisiri kuwa mfalme (4-12)

  • Athalia auawa (13-16)

  • Mabadiliko yaliyofanywa na Yehoyada (17-21)

11  Basi Athalia+ mama ya Ahazia alipoona kwamba mwanawe amekufa,+ alitoka na kuangamiza uzao wote wa kifalme.*+  Hata hivyo, Yehosheba binti ya Mfalme Yehoramu, dada ya Ahazia, akamchukua Yehoashi+ mwana wa Ahazia, akamwiba kutoka miongoni mwa wana wa mfalme waliopaswa kuuawa na kumweka yeye pamoja na mlezi wake katika chumba cha ndani cha kulala. Wakafanikiwa kumficha ili Athalia asimwone, kwa hiyo hakuuawa.  Akakaa pamoja naye kwa miaka sita akiwa amefichwa katika nyumba ya Yehova, Athalia alipokuwa akitawala nchi.  Katika mwaka wa saba, Yehoyada aliagiza wakuu wa mamia wa walinzi walioitwa Wakari na wa walinzi* wa jumba la mfalme+ waitwe, wakaja kwake katika nyumba ya Yehova. Akafanya mapatano* pamoja nao na kuwaapisha kuhusu mapatano hayo katika nyumba ya Yehova, kisha akawaonyesha mwana wa mfalme.+  Akawapa agizo hili: “Hivi ndivyo mtakavyofanya: Theluthi moja watashika zamu siku ya Sabato, na kuweka ulinzi mkali katika nyumba ya* mfalme,+  theluthi nyingine watakuwa katika Lango la Msingi, na theluthi nyingine watakuwa katika lango lililo nyuma ya walinzi wa jumba la mfalme. Mtalinda nyumba hiyo kwa zamu.  Vikundi vyenu viwili ambavyo havipaswi kuwa na zamu siku ya Sabato vinapaswa kuweka ulinzi mkali katika nyumba ya Yehova ili kumlinda mfalme.  Mnapaswa kumzunguka mfalme pande zote, kila mmoja akiwa na silaha zake mikononi mwake. Yeyote atakayekaribia kikosi hicho atauawa. Mfuateni mfalme popote aendapo.”*  Wakuu wa mamia+ wakafanya sawasawa na alivyoamuru kuhani Yehoyada. Basi kila mmoja wao akachukua wanaume wake waliokuwa na zamu siku ya Sabato, pamoja na wale ambao hawakuwa na zamu siku ya Sabato, wakaja kwa kuhani Yehoyada.+ 10  Kisha kuhani akawapa wakuu wa mamia mikuki na ngao za mviringo zilizokuwa za Mfalme Daudi, ambazo zilikuwa katika nyumba ya Yehova. 11  Na walinzi wa jumba la mfalme+ wakasimama mahali pao, kila mmoja akiwa na silaha zake mikononi, kuanzia upande wa kulia wa nyumba mpaka upande wa kushoto wa nyumba, kando ya madhabahu,+ na kando ya nyumba hiyo, kumzunguka mfalme pande zote. 12  Kisha Yehoyada akamtoa nje mwana wa mfalme+ na kumvika taji na Ushahidi,*+ wakamweka kuwa mfalme na kumtia mafuta. Wakaanza kupiga makofi na kusema: “Mfalme na aishi muda mrefu!”+ 13  Athalia aliposikia sauti ya watu wakikimbia, mara moja akaja na kujiunga na watu katika nyumba ya Yehova.+ 14  Kisha akamwona mfalme akiwa amesimama hapo kando ya nguzo kama ilivyokuwa desturi.+ Wakuu na wapiga tarumbeta+ walikuwa pamoja na mfalme, na watu wote nchini walikuwa wakishangilia na kupiga tarumbeta. Ndipo Athalia akayararua mavazi yake na kupaza sauti: “Ni njama! Ni njama!” 15  Lakini kuhani Yehoyada akawaamuru hivi wakuu wa mamia,+ wale waliowekwa kulisimamia jeshi: “Mwondoeni miongoni mwa vikosi, na yeyote akimfuata, muueni kwa upanga!” Kwa maana kuhani alikuwa amesema: “Msimuue ndani ya nyumba ya Yehova.” 16  Basi wakamkamata, na alipofika mahali ambapo farasi huingia katika nyumba ya* mfalme,+ akauawa hapo. 17  Kisha Yehoyada akafanya agano kati ya Yehova na mfalme na watu,+ kwamba wataendelea kuwa watu wa Yehova, pia akafanya agano kati ya mfalme na watu.+ 18  Baada ya hayo, watu wote nchini wakaenda kwenye nyumba ya* Baali na kubomoa madhabahu zake,+ nao wakazivunja kabisa sanamu zake,+ na kumuua Matani kuhani wa Baali+ mbele ya madhabahu. Halafu kuhani akawaweka waangalizi wa nyumba ya Yehova.+ 19  Tena, akawachukua wakuu wa mamia,+ walinzi walioitwa Wakari, walinzi wa jumba la mfalme,+ na watu wote nchini ili wamsindikize mfalme kushuka kutoka katika nyumba ya Yehova, wakaja katika jumba la mfalme kupitia lango la walinzi wa jumba la mfalme. Kisha mfalme akaketi kwenye kiti cha wafalme.+ 20  Basi watu wote nchini wakashangilia na jiji likatulia, kwa maana walikuwa wamemuua Athalia kwa upanga katika jumba la mfalme. 21  Yehoashi+ alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “mbegu yote ya ufalme.”
Tnn., “wakimbiaji.”
Au “agano.”
Au “jumba la.”
Tnn., “anapotoka nje na anapoingia ndani.”
Labda ni kitabu cha kukunjwa kilichokuwa na Sheria ya Mungu.
Au “jumba la.”
Au “hekalu la.”