Barua ya Pili kwa Wathesalonike 2:1-17
2 Hata hivyo, akina ndugu, kuhusu kuwapo kwa Bwana wetu Yesu Kristo+ na kukusanywa kwetu pamoja kwake,+ tunawaomba
2 msitikiswe upesi kutoka kwenye kufikiri kwenu wala msitishwe na maneno yaliyoongozwa na roho*+ au ujumbe uliosemwa au barua inayodhaniwa kutoka kwetu, kwamba siku ya Yehova*+ imefika.
3 Msiruhusu mtu yeyote awapotoshe* kwa njia yoyote, kwa sababu siku hiyo haitafika kabla uasi imani+ haujatokea kwanza na yule mtu wa uasi sheria+ kufunuliwa, mwana wa maangamizi.+
4 Yeye ni mpinzani na hujiinua juu ya wale wanaoitwa mungu au vitu vinavyoabudiwa,* na hivyo huketi katika hekalu la Mungu, akijionyesha waziwazi kuwa mungu.
5 Je, hamkumbuki kwamba nilikuwa nikiwaambia mambo hayo nilipokuwa pamoja nanyi?
6 Sasa mnajua kinachomzuia, ili afunuliwe wakati wake unaofaa.
7 Kwa kweli, fumbo la uasi sheria huu tayari linafanya kazi,+ lakini ni mpaka tu yule anayeuzuia sasa atakapoondolewa.
8 Ndipo, kwa kweli, yule mwasi sheria atafunuliwa, ambaye Bwana Yesu atamwangamiza kwa roho ya kinywa chake+ na kumharibu kupitia ufunuo+ wa kuwapo kwake.
9 Lakini kuwapo kwa huyo mwasi sheria ni kupitia kazi ya Shetani+ pamoja na kila tendo lenye nguvu na ishara za uwongo na mambo ya ajabu*+
10 na kila namna ya udanganyifu usio wa uadilifu+ kwa wale wanaoangamia, kama malipo kwa sababu hawakukubali kuipenda kweli ili waokolewe.
11 Ndiyo sababu Mungu anaacha wapotoshwe kupitia udanganyifu, na hivyo waamini uwongo,+
12 ili wote wahukumiwe kwa sababu hawakuiamini kweli, bali walipenda ukosefu wa uadilifu.
13 Hata hivyo, tuna wajibu wa kumshukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu akina ndugu mnaopendwa na Yehova,* kwa sababu tangu mwanzo Mungu aliwachagua+ ili mwokolewe kwa kuwatakasa+ kupitia roho yake na imani yenu katika kweli.
14 Aliwaita kupitia habari njema tunayotangaza, ili mpate utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.+
15 Basi, akina ndugu, simameni imara+ na mwendelee kufuata desturi mlizofundishwa,+ iwe ni kupitia ujumbe wa maneno au barua kutoka kwetu.
16 Zaidi ya hayo, Bwana wetu Yesu Kristo, na Mungu Baba yetu aliyetupenda+ na kutupatia faraja ya milele na tumaini jema+ kupitia fadhili zisizostahiliwa,
17 na aifariji mioyo yenu na kuwaimarisha* katika kila tendo na neno jema.
Maelezo ya Chini
^ Angalia Nyongeza A5.
^ Au “awashawishi.”
^ Au “vinavyoheshimiwa.”
^ Au “miujiza.”
^ Angalia Nyongeza A5.
^ Au “kuwatia nguvu.”